-
UNICEF: Zaidi ya nusu ya wakimbizi barani Afrika ni watoto wadogo
Jul 05, 2017 08:14Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umesema kuwa, zaidi yawatoto milioni saba wa maeneo ya magharibi na katikati mwa Afrika wanaishi katika mazingira magumu kutokana na matatizo mbalimbali kama vile ukatili, umaskini na kuharibika hali ya hewa na kwamba idadi hiyo inaunda zaidi ya nusu ya wakimbizi barani Afrika.
-
Afghanistan yatoa shukurani kwa Iran kwa kuwahifadhi wakimbizi wa nchi hiyo
Jun 21, 2017 02:44Mkuu wa Baraza la Utekelezaji la Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Afghanistan, Abdullah Abdullah ametoa shukurani za dhati kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuwapa hifadhi maelfu ya wakimbizi wa taifa hilo katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita.
-
Makumi ya wahajiri wahofiwa kufa maji pwani ya Libya
Jun 11, 2017 14:09Makumi ya wahajiri wanahofiwa kufa maji baada ya boti yao kuzama mashariki mwa Tripoli, mji mkuu wa Libya.
-
Miili 7 ya wahajiri wa Kiafrika yapatikana ndani ya lori Libya
Jun 05, 2017 14:06Wahajiri saba wa Kiafrika wamepoteza maisha baada ya kukosa hewa wakiwa ndani ya lori lenye jokofu kwa muda wa siku mbili katika pwani ya Libya.
-
IOM: Wanaofanya magendo ya wahajiri wanapata dola bilioni 35 kwa mwaka
Jun 01, 2017 03:20Shirika la Wahajiri Duniani IOM limesema watu wanaofanya biashara haramu ya magendo ya wahajiri wanatengeneza faida ya dola bilioni 35 za Marekani kila mwaka.
-
Wahajiri 58 wafa maji bahari ya Mediterrania, 100 watoweka
May 30, 2017 15:33Umoja wa Mataifa umesema wahajiri 58 aghalabu yao wakiwa ni watoto wadogo wamekufa maji katika Bahari ya Mediterrania karibu na pwani ya Libya wakijaribu kuingia barani Ulaya.
-
Mfululizo wa vipindi vya 'Ukatili wa Mabudha dhidi ya Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar' na Sauti
May 28, 2017 11:23Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wapenzi wasikilizaji na karibuni kutegea sikio sehemu ya saba ya makala yanayozungumzia jinai na ukatili wa kutisha unaofanywa na Mabudha wenye kuchupa mipaka dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya nchini Myanmar.
-
Wahajiri 34, aghlabu yao watoto, wazama baharini Libya
May 25, 2017 04:27Wahajiri wasiopungua 34, wengi wao wakiwa ni watoto, walizama jana Jumatano katika Bahari ya Mediterranean karibu na pwani a Libya.
-
Wahajiri haramu 4400 waokolewa katika maji ya Mediterranean siku mbili pekee
May 20, 2017 07:24Duru za habari nchini Libya zimetangaza kuwa kikosi cha gadi ya pwani ya Libya na Italia kimefanikiwa kuokoa karibu wahajiri haramu 400 katika kipindi cha siku mbili kutoka katika maji ya bahari ya Mediterranean.
-
HRW yakosoa muswada wa sheria dhidi ya wahamiaji Marekani
May 19, 2017 07:41Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limekosoa vikali muswada uliopendekezwa na serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani, ambao ukipasishwa na kuwa sheria basi vyombo vya dola vitaongezewa nguvu na mamlaka ya kuwabana zaidi wahamiaji haramu nchini humo.