-
Wanahabari wa Afrika waunda Muungano wa Kupinga Mauaji ya Kimbari ya Israel Gaza
Aug 24, 2025 23:29Waandishi wa habari kutoka bara zima la Afrika wamezindua muungano uliopewa jina la 'African Journalists Against Genocide (AJAG)' wenye lengo la kupinga kile wanachoeleza kuwa ni mauaji ya kimbari ya Israel na uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Gaza, wakiwemo wanahabari wenzao.
-
TICAD inaimarisha vipi nafasi ya Afrika katika siasa na uchumi wa dunia?
Aug 24, 2025 23:01Mkutano wa 9 wa Kimataifa wa Maendeleo ya Afrika, Tokyo International Conference on African Development (TICAD), ulimalizika Ijumaa, Agosti 22 kwa kusainiwa mikataba takriban 300 ya ushirikiano kati ya taasisi za Japan na Afrika kuhusu masuala mbalimbali ya afya, teknolojia, elimu, kilimo, maendeleo ya miundombinu na ujenzi wa miundomsingi.
-
Serikali ya Eswatini inakabiliwa na kesi mahakamani kuhusu watu waliofukuzwa Marekani
Aug 24, 2025 07:24Kundi la mawakili watetezi wa haki za binadamu na taasisi zisizo na kiserikali (NGOs) linaishtaki serikali ya Eswatini kwa kukubali kuwapa hifadhi watu watano waliofukuzwa nchini Marekani.
-
Watu 46 wapoteza maisha kutokana na njaa katika jimbo la Kordofan nchini Sudan
Aug 24, 2025 04:30Angalau watu 46, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wamefariki kutokana na njaa nchini Sudan katika jimbo la Kordofan Kusini katika kipindi cha miezi miwili iliyopita. Hayo yamedokezwa na Shirika la Madaktari wa Sudan huku eneo hilo lenye vita likikumbwa na njaa kali na uhaba wa dawa.
-
Chanjo kutoka Afrika: Matumaini yapatikana
Aug 23, 2025 23:25Tangu janga la Corona (UVIKO-19), Afrika imezindua mipango ya kutengeneza chanjo na dawa kwa ajili ya kuboresha huduma za afya. Ingawa mafanikio ya awali yanaonekana, lakini bado kunahitajika ufadhili wa muda mrefu.
-
UN: DRC inakabiliwa na moja ya hali mbaya zaidi za kibinadamu duniani
Aug 23, 2025 06:06Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliana na mojawapo ya majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani, huku machafuko na ukosefu wa usalama vikiendelea kuwaangamiza raia mashariki mwa nchi hiyo.
-
Uganda yaafiki kuwapokea wahamiaji waliotimuliwa Marekani kama hawana rekodi za uhalifu
Aug 23, 2025 06:01Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema, nchi hiyo itakubaliana na mpango wa Marekani wa kuwapokea wahamiaji waliofukuzwa nchini humo ikiwa hawatakuwa na rekodi za uhalifu au si watoto wasio na jamaa zao.
-
Mwendesha mashtaka wa DRC ataka Kabila ahukumiwe kifo
Aug 23, 2025 02:45Mwendesha mashtaka wa kijeshi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametoa mwito wa kutolewa hukumu ya kifo dhidi ya rais wa zamani wa nchi hiyo, Joseph Kabila ambaye mashitaka dhidi yake yanaendelea bila ya yeye kuwepo mahakamani.
-
Shambulizi la droni Sudan lateketeza malori 16 ya Umoja wa Mataifa
Aug 23, 2025 00:27Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, shambulizi la droni katika msafara umesababisha kuteketea kwa malori 16 ya misaada iliyokuwa inahitajika mno katika eneo la Darfur Kaskazini nchini Sudan, lililokumbwa na uhaba mkubwa wa chakula.
-
Viwiliwili visivyopungua vitano vya wahanga wa itikadi kali za kidini vyafukuliwa Kenya
Aug 22, 2025 08:20Viwiliwili visivyopungua vitano vimefukuliwa kutoka kwenye makaburi yenye kina kifupi katika eneo moja la pwani kaskazini ya Kenya, ambako wahanga wa itikadi kali za kidini wanashukiwa kuwa walizikwa.