-
Jeshi la Somalia laua zaidi ya magaidi 37 wa al-Shabaab
Jun 30, 2025 08:00Kikosi maalum cha Danab cha Jeshi la Somalia kimewaua zaidi ya wanamgambo 37 wa kundi la al-Shabaab katika kijiji cha Maqooqaha, kilichoko magharibi mwa Buulo Xaaji katika eneo la Lower Jubba, kusini mwa nchi.
-
Watoto zaidi ya 239 wafariki magharibi mwa Sudan kwa njaa na ukosefu wa dawa
Jun 30, 2025 07:52Watoto wasiopungua 239 wamefariki dunia katika eneo la magharibi mwa Sudan tangu Januari mwaka huu kutokana na ukosefu wa chakula na dawa, kwa mujibu wa taarifa ya Mtandao wa Madaktari wa Sudan iliyotolewa Jumapili.
-
Watu 7 wauawa katika maandamano ya siku mbili huko Togo dhidi ya Rais Gnassingbe
Jun 30, 2025 04:31Mashirika ya haki za binadamu na taasisi za kiraia zimeripoti kuwa watu wasiopungua saba wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika maandamano dhidi ya serikali katika mji mkuu wa Togo, Lome. Watu hao waliuawa katika maandamano yaligeuka na kuwa ghasia kuanzia Alhamisi hadi juzi Jumamosi.
-
Takriban watoto 239 wamefariki dunia magharibi mwa Sudan tangu Januari
Jun 30, 2025 04:30Takriban watoto 239 wameaga dunia magharibi mwa Sudan tangu mwezi Januari mwaka huu kutokana na ukosefu wa chakula na dawa za kutosha. Ripoti hii imetolewa na Mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Ajali mbaya ya barabarani yaua watu 38 nchini Tanzania
Jun 30, 2025 00:54Watu 38 wameripotiwa kufariki dunia na wengine 30 wamejeruhiwa nchini Tanzania baada ya mabasi mawili kugongana na kuwaka moto.
-
Watu takribani 50 wafariki baada ya kuporomoka mgodi wa dhahabu Sudan
Jun 29, 2025 10:44Takriban watu 50 wamefariki dunia kufuatia kuporomoka kwa mgodi wa dhahabu kaskazini mashariki mwa Sudan, vyombo vya habari vya ndani vimeripoti Jumapili.
-
Museveni achukua fomu ya kuwania muhula wa saba madarakani
Jun 28, 2025 23:14Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameomba tena uteuzi wa kugombea muhula wa saba, hatua inayomuelekeza kwenye miaka 50 ya kuwa madarakani.
-
Chama cha DA cha Afrika Kusini chajiondoa kwenye mazungumzo ya kitaifa
Jun 28, 2025 23:14Chama cha Democratic Alliance cha nchini Afrika Kusini kimejiondoa kwenye mazungumzo ya kitaifa hata hivyo hakijajitoa katika serikali ya mseto baada ya Rais wanchi hiyo Cyril Ramaphosa kumfuta kazi Naibu Waziri wake mmoja. Haya yameelezwa na kiongozi wa chama hicho John Steenhuisen.
-
EACC: Wanafunzi Kenya wanatumiwa na viongozi kusajili kampuni hewa za kupora pesa
Jun 28, 2025 04:58Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi ya Kenya (EACC) imefichua mpango, ambapo maafisa wa juu wa serikali za Kaunti, wakiwemo magavana wanadaiwa kuwahusisha wanafunzi walioko kwenye mafunzo ya kazi kama njia ya kufuja mabilioni ya pesa za umma kupitia kampuni hewa.
-
Amnesty Kenya: Vifo 16 vimesajiliwa kufuatia ghasia zilizojiri nchini
Jun 26, 2025 12:20Watu 16 wameuawa na mamia wamejeruhiwa wakati wa maandamano ya kitaifa dhidi ya serikali nchini Kenya siku ya Jumatano, ambapo kwa mujibu wa Mkuu wa shirika la Amnest Kenya na Kamisheni ya Taifa ya Kenya ya Haki za Binadamu, wengi wao wameuawa na polisi.