-
Afrika imenakili vifo 4,200 vya kipindupindu na mpox 2025
Jul 12, 2025 09:22Afrika imerekodi vifo zaidi ya 4,200 kutokana na miripuko ya kipindupindu na mpox inayoendelea kuripotiwa katika maeneo tofauti ya bara hilo mwaka 2025, Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) kimesema.
-
Mwanaharakati: Mkataba wa Uvuvi kati ya Gambia na EU ni "Mkataba Mbovu Zaidi wa Uvuvi"
Jul 12, 2025 04:19Mwanaharakati maarufu kutoka Gambia, magharibi mwa Afrika amesema kuwa mkataba wa uvuvi kati ya nchi hiyo na Umoja wa Ulaya (EU) ni "mkataba mbaya kabisa wa uvuvi" kuwahi kushuhudiwa.
-
Uchaguzi wa rais Cameroon kufanyika mwezi Oktoba
Jul 12, 2025 04:08Serikali ya Cameroon imetangaza kuwa uchaguzi wa urais utafanyika tarehe 12 Oktoba. Hayo ni kwa mujibu wa amri iliyosainiwa Ijumaa na Rais Paul Biya.
-
Nigeria: US inazilazimisha nchi za Afrika ziwapokee wakimbizi Wavenezuela
Jul 11, 2025 13:11Nigeria imefichua kuwa Marekani inazishinikiza nchi za bara Afrika kuwakubali wakimbizi wa Venezuela wanaofukuzwa nchini Marekani.
-
Magaidi 13 wa al-Shabaab wauawa katika operesheni ya jeshi Somalia
Jul 11, 2025 12:25Shirika la kitaifa la ujasusi na usalama la Somalia (NISA) jana Ijumaa lilisema kuwa lmeifanya operesheni tatu zilizoratibiwa katika eneo la Shabelle ya Kati, na kuua takriban wanachama 13 wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab, wakiwemo wapiganaji na makamanda wake.
-
ICC: Uhalifu wa kivita, jinai dhidi ya binadamu vinaendelea Darfur, Sudan
Jul 11, 2025 11:23Naibu Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC amesema kuna "sababu za kuamini kwamba uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu" unaendelea kufanywa katika eneo la magharibi mwa Sudan la Darfur,
-
Mufti wa Misri alaani ziara ya ‘mashekhe wa Ulaya’ waliotembelea Israel
Jul 11, 2025 10:08Mufti wa Misri, Sheikh Nazir Ayad, amelaani ziara iliyofanywa na kundi alilolitaja kama "wale wanaojitangaza kuwa shakhsia wa kidini", waliotembelea ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu zilizopachikwa jina bandia la Israel na kuitaja ziara hiyo kuwa ni "uwekezaji wa bei rahisi wa kisiasa kwa kutumia majoho bandia ya ushekhe ili kuipamba sura ya utawala ghasibu wa umwagaji damu".
-
Kauli ya Trump ya “Kiingereza kizuri” yawakasirisha Waafrika, yazua mdahalo kuhusu ukoloni mamboleo
Jul 11, 2025 04:13Watu wa Liberia na Waafrika kwa ujumla wameonyesha hasira baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kuwa alishangazwa na jinsi rais wa Liberia anavyoongea “Kiingereza kizuri.” Kauli hiyo imeibua wimbi la ukosoaji kote Afrika.
-
DRC yaendelea kupambana na mlipuko wa kipindupindu
Jul 11, 2025 04:12Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) inaendelea kukabiliana na kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa kipindupindu, ambapo visa vilivyothibitishwa vimefikia 1,601 kote.
-
IOM: Mamia ya familia za raia wa Sudan watoroka Kordofan kutoka na vita
Jul 10, 2025 17:36Mapigano kati ya jeshi la Sudan na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yamelazimisha familia 700 kulikimbia Jimbo la Kordofan Kaskazini, huko kusini mwa Sudan, Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) lilisema hayo jana Alkhamisi.