-
Uganda yatangaza kumalizika mripuko wa karibuni wa ugonjwa wa Ebola
Apr 26, 2025 23:02Uganda imetangaza kumalizika mripuko uliozuka karibuni zaidi wa ugonjwa wa Ebola miezi mitatu baada ya mamlaka husika kuthibitisha kesi za maambukizo ya ugonjwa huo katika mji mkuu Kampala.
-
Nchi zenye wanajeshi wa AU zataka kuimarishwa usalama Somalia
Apr 26, 2025 07:39Mawaziri wa ulinzi na mambo ya nje wa nchi zenye wanajeshi katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika (AU) nchini Somalia wametoa mwito wa kuchukuliwa hatua za haraka za kuongeza idadi ya wanajeshi na kuimarisha usalama nchini Somalia kutokana na kuzidi kudorora hali ya usalama huku genge la kigaidi la al-Shabaab likizidi kuimarika.
-
UN yataka kukomeshwa mapigano mara moja Sudan Kusini
Apr 26, 2025 07:38Timu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS imetoa mwito wa kukomeshwa mara moja mapigano baada ya kushadidi vita kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) na wanajeshi wa upinzani wanaomuunga mkono Makamu wa Kwanza wa Rais, Riek Machar.
-
Jeshi la Msumbiji laokoa wanawake 280 na watoto kutoka mikononi mwa wanamgambo wa Naparama
Apr 26, 2025 07:37Jeshi la Msumbiji limesema kuwa limefanikiwa kuokoa wanawake na watoto wasiopungua 280 waliokuwa wametekwa nyara na wanamgambo wa Naparama katika majimbo ya kaskazini na katikati mwa nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Afrika.
-
UN yatahadharisha kuhusu hali mbaya za wakimbizi wa Kongo wanaoingia Burundi
Apr 26, 2025 03:04Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limesema kuongezeka idadi ya wakimbizi wanaokimbia mzozo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenda Burundi kunaweka "shinikizo kubwa kwa mashirika ya misaada yanayojitahidi kukabiliana na mzozo unaozidi kuwa mbaya huku kukiwa na uhaba wa rasilimali."
-
RSF yaendelea kuua raia Sudan, UN yasema milioni 13 wamelazimika kukimbia makazi yao
Apr 25, 2025 10:17Mtandao wa Madaktari wa Sudan umesema watu 11 wameuawa na 22 kujeruhiwa wakati ndege isiyo na rubani ya Rapid Support Forces (RSF) iliposhambulia kambi ya wakimbizi huko Atbara, kaskazini mwa Sudan.
-
UN: Hukumu ya kesi ya "uhaini" nchini Tunisia ni pigo kwa haki na uadilifu
Apr 25, 2025 09:09Umoja wa Mataifa umetaja hukumu zilizotolewa dhidi ya makumi ya watu wakiwemo viongozi wa upinzani katika kesi ya "njama dhidi ya usalama wa taifa" nchini Tunisia kuwa ni "kurudisha nyuma haki na utawala wa sheria," ukieleza kuwa kulikuwa na "matashi ya kisiasa" nyuma ya maamuzi hayo.
-
Mtaalamu wa sheria Kenya: Uchaguzi wa rais unapaswa kufanyika 2026 na sio 2027 kama ilivyopangwa
Apr 25, 2025 08:09Mtaalamu wa sheria ya uchaguzi wa Kenya amesema kuwa uchaguzi mkuu ujao unapasa kufanyika 2026 na sio 2027.
-
Kutoweza Afrika Kusini kuachana na Muqawama na ukombozi wa Palestina
Apr 25, 2025 03:47Tarehe 29 Disemba 2023 imerekodiwa katika kumbukumbu za historia ya baada ya mwaka 1994 ya Afrika Kusini kama siku muhimu sana baada ya Pretoria kufungua kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika mahakama ya ICJ, ikiwasilisha hoja za kisheria za kina na zenye mashiko kwamba ukatili wa Israel katika Ukanda wa Ghaza unakanyaga Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia Mauaji ya Kimbari.
-
Jeshi la Msumbiji: Uasi katika mkoa wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado umemalizika
Apr 25, 2025 03:12Jeshi la Msumbiji limetangaza kuwa limedhibiti kambi za mwisho za mafunzo zilizokuwa zikitumiwa na waasi katika mkoa wa kaskazini wa Cabo Delgado, ikiwa ni ishara ya kile wanachokitaja maafisa wa jeshi hilo kuwa ni kumalizika kwa uasi wa miaka mingi katika eneo hilo lenye utajiri wa maliasili ya gesi.