-
Mali: Muungano wa Mataifa ya Sahel umevuruga nguvu za ukoloni
Apr 04, 2025 06:41Waziri wa Mambo ya Nje wa Mali, Abdoulaye Diop, amesema kuwa Muungano wa Mataifa ya Sahel (AES) ulioundwa na Mali, Niger na Burkina Faso mwaka 2023, umebadili kabisa mlingano wa nguvu za kimkakati kwa madola ya kikoloni ambayo yanataka kuendelea kutawala nchi hizo.
-
Afrika Kusini iliwafukuza karibu wahamiaji haramu 47,000 mwaka wa fedha wa 2024/25.
Apr 04, 2025 03:33Wizara ya Mambo ya Ndani ya Afrika Kusini imetoa ripoti mpya na kusema kuwa, Pretoria iliwafukuza wahamiaji haramu 46,898 mwaka wa fedha wa 2024/25.
-
Afrika Kusini yaonya kuhusu vita vipya vya ushuru vya Trump
Apr 03, 2025 23:44Jana Alkhamisi, Afrika Kusini ilionya kuhusu vita vipya vya ushuru vilivyoanzishwa na rais wa Marekani na kuelezea wasiwasi wake kuhusu ushuru uliowekwa na Donald Trump kwa bidhaa za Afrika Kusini na kusema hilo litakuwa na madhara kwa pande zote mbili.
-
Deni la serikali ya Namibia limeongezeka kwa asilimia 10
Apr 03, 2025 23:39Katika ripoti yake ya karibuni kabisa, Benki Kuu ya Namibia imetangaza kwamba, deni la serikali ya nchi hiyo limepanda na kufikia dola bilioni 164 za Namibia (kama dola bilioni 8.8 za Kimarekani) mwishoni mwa Desemba 2024 suala ambalo linaashiria ongezeko la asilimia 10.2 la deni hilo tangu mwanzoni mwa mwaka wa fedha wa 2024/25.
-
Wakala wa hali ya hewa watabiri mvua kubwa na hatari za mafuriko mashariki mwa Afrika
Apr 03, 2025 23:39Kituo cha Utabiri wa Hali ya Hewa na Maombi (ICPAC) cha Mamlaka ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD), kambi ya kikanda, kimetangaza kuwa, nchi kadhaa za mashariki na Pembe ya Afrika zinatazamiwa kupata mvua nyingi kuliko kawaida katika siku zijazo, na hivyo kusababisha mafuriko.
-
Kwa nini Rais Mnangagwa wa Zimbabwe anakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu?
Apr 03, 2025 08:05Mgawanyiko unaendelea kushuhudiwa ndani wa chama tawala cha ZANU-PF nchini Zimbabwe umeibua hofu ya uwezekano wa jaribio la mapinduzi dhidi ya Rais Mnangagwa, ambaye anajaribu kusalia madarakani baada ya mwaka 2028 licha ya kuwa ni kinyume na katiba.
-
Bunge la Msumbiji lapasisha sheria kuhusu mazungumzo ya kitaifa ili kurejesha amani
Apr 03, 2025 08:04Bunge la Msumbiji kwa kauli moja limepaisha sheria ili kurejesha amani katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika kufuatia miezi kadhaa ya maandamano makubwa ya ghasia ya wananchi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika Oktoba 9. Watu takriban 360 walipoteza maisha katika maandamano hayo ya ghasia.
-
Watu 89 wauawa katika mashambulizi ya RSF Omdurman, Sudan
Apr 03, 2025 03:36Raia wasiopungua 89 wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa katika mashambulizi ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kwenye vijiji vya Omdurman, karibu na ufukwe wa Mto Nile, kaskazini magharibi mwa Khartoum, mji mkuu wa Sudan.
-
RSF yaua na kujeruhi makumi ya raia wa Sudan Kordofan Kusini
Apr 02, 2025 23:02Kwa akali raia 12 wa Sudan wameuawa katika mashambulizi ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) katika Jimbo la Kordofan Kusini.
-
Serikali ya DRC na waasi wa M23 kufanya mazungumzo ya kwanza Aprili 9 nchini Qatar
Apr 02, 2025 07:08Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imepanga kufanya mazungumzo ya kwanza kabisa na kundi la waasi wa M23, April 9 mwaka huu katika mji mkuu wa Qatar, Doha kwa lengo la kufikia mwafaka wa kurejesha amani katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo.