-
Watu 71 wafariki dunia baada ya basi la sherehe ya harusi kutumbukia mtoni nchini Ethiopia
Dec 30, 2024 08:51Takriban watu 71 wamepoteza maisha nchini Ethiopia baada ya basi lililokuwa limebeba abiria lililpoacha njia na kutumbukia mtoni. Haya yameelezwa na msemaji wa serikali ya jimbo la Sidama kusini mwa Ethiopia.
-
Sudan: Vyombo vya habari vya Magharibi vinapotosha ukweli kuhusu vita
Dec 30, 2024 08:50Waziri wa Habari na Utamaduni wa Sudan amevituhumu vyombo vya habari vya Magharibi kwa kupotosha uhakika wa mambo kuhusiana na vita vinavyoendelea nchini humo akisema kuwa vyombo hivyo vinaegemea upande wa kikosi cha RSF.
-
Senegal; kituo kinachofuata cha kufukuzwa wanajeshi wa Ufaransa barani Afrika
Dec 30, 2024 04:42Ousmane Sonko,Waziri Mkuu wa Senegal amewaambia wabunge wa nchi hiyo kwamba wanajeshi wa Ufaransa lazima waondoke nchini humo na kwamba, kambi za kijeshi za kigeni katika nchi hiyo ya Kiafrika zitafungwa katika siku za usoni.
-
Watu wa Chad wanasubiri matokeo ya uchaguzi wa bunge
Dec 30, 2024 04:22Wananchi wa Chada Jumapili walishiriki katika uchaguzi wa kwanza wa bunge baada ya miaka 13, ambao serikali imeutaja uchaguzi huo kama hatua muhimu kuelekea kumaliza utawala wa kijeshi.
-
Rais wa Algeria akosoa Ufaransa kuhusu historia yake ya ukoloni
Dec 30, 2024 04:21Rais wa Algeria Abdelmadjid Tebboune amekosoa vikali Ufaransa kuhusu athari za utawala wake wa kikoloni zilizosalia nchini humo.
-
Wanamgambo wanaosaidiwa na UAE washambulia makazi ya raia nchini Sudan, waua watu 21
Dec 29, 2024 23:35Wanamgambo wanaoungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) wameshambulia makazi ya raia magharibi mwa Sudan na kuua watu 21 waliokimbia makazi huko.
-
Rais wa Misri afuatilia kwa makini makubaliano ya Ethiopia na Somalia
Dec 29, 2024 23:32Rais wa Misri, Abdel Fattah al-Sisi, amesema anafuatilia kwa karibu makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Ethiopia na Somalia kwa upatanishi wa Uturuki.
-
Waasi wa ADF waua raia wasiopungua 21 mashariki ya DRC katika wiki ya Krismasi
Dec 29, 2024 07:31Waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) wameua watu wasiopungua 21 katika mashambulio kadhaa waliyofanya katika wiki ya Krismasi kwenye eneo lililokumbwa na mgogoro wa vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Uchunguzi wa WHO washindwa kubaini ugonjwa wa ajabu DRC
Dec 29, 2024 04:13Uchunguzi uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) umeshindwa kubaini ugonjwa wa ajabu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao hadi sasa umeua makumi ya watu.
-
Al-Azhar yalaani unyama wa Israel wa kuchoma moto hospitali ya Kamal Adwan
Dec 29, 2024 03:48Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al-Azhar cha nchini Misri kimelaani vikali hatua ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuchoma moto na kuharibiwa kabisa Hospitali ya Kamal Adwan huko Gaza.