-
Kwa nini ni muhimu Ulimwengu wa Kiislamu kuchukua msimamo mmoja dhidi ya utawala wa Kizayuni?
Apr 05, 2025 22:49Katika muendelezo wa sera za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran za kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na ulazima wa Ulimwengu wa Kiislamu kuzingatia hali ya Ghaza, Ali Akbar Velayati, Katibu Mkuu wa Baraza la Kimataifa la Mwamko wa Kiislamu ametoa taarifa ya kulaani hujuma za kinyama za utawala vamizi wa Kizayuni dhidi ya wananchi wanaodhulumiwa wa Ghaza na wa kusini mwa Lebanon.
-
Rais wa Iran amfuta kazi Makamu wake kwa 'safari ya ubadhirifu'
Apr 05, 2025 06:07Rais Masoud Pezeshkian amempiga kalamu nyekundu Makamu wake katika Masuala ya Bunge kufuatia safari ya kibinafsi ya mwanasiasa huyo wakati wa sherehe za mwaka mpya wa Kiirani (Nowruz), iliyojaa ubadhirifu.
-
Abu Turabi Fard: Jamii ya Kiislamu inakabiliwa na mtihani mkubwa katika kulihami taifa la Palestina
Apr 04, 2025 09:01Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo mjini Tehran amesema, Jamii ya Kiislamu inakabiliwa na mtihani mkubwa katika kulihami taifa adhimu la Palestina na kusimama imara kukabiliana na Uistikbari na mamluki wake yaani utawala wa niaba wa Wazayuni katika eneo hili.
-
Kuwa tayari Iran kuimarisha ushirikiano na nchi za eneo
Apr 04, 2025 06:57Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na wakuu wa baadhi ya nchi za eneo na kusisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuimarisha uhusiano na ushirikiano na nchi hizo katika nyanja mbalimbali kwa mujibu wa imani na itikadi za Kiislamu.
-
Pezeshkian: Ikiwa Waislamu wataungana, maadui hawawezi kuyadhulumu mataifa ya Kiislamu
Apr 04, 2025 06:47Rais wa Iran amesema kuwa ikiwa Waislamu watakuwa na umoja na mshikamano, maadui hawatakuwa na uwezo wa kuyadhulumu mataifa ya Kiislamu.
-
Iran yalalamikia vikali azimio la Baraza la Haki za Binadamu la UN
Apr 04, 2025 06:45Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Geneva amekosoa vikali kupitishwa kwa azimio la kupinga Iran katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, akilitaja kuwa ni kitendo cha kibaguzi na kinachopunguza itibari wa baraza hilo.
-
Rais Pezeshkian: Iran haiko vitani na nchi yoyote
Apr 04, 2025 03:35Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudia na kusisitiza kwa kusema: "Nina imani kwamba kama nchi za Kiislamu zitafanya kazi kwa pamoja, zinaweza kuleta usalama na ustawi bora katika eneo hili."
-
Iran yalaani mashambulizi la Israel dhidi ya miundombinu ya raia na ulinzi ya Syria
Apr 04, 2025 03:34Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje amelaani vikali hujuma ya kijeshi ya anga na ardhini ya utawala wa wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Syria na uharibifu wa vituo vya utafiti vya kiraia na kisayansi, pamoja na mlolongo wa miundombinu ya ulinzi ya nchi hiyo katika majimbo ya Damascus, Hama, Homs na Daraa.
-
SEPAH: Muqawama utakomesha uwepo mchafu wa utawala wa Kizayuni
Apr 03, 2025 23:44Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la nchini Iran SEPAH limetoa taarifa na kutangaza kuwa: "Kambi ya Muqawama hususan wanamapambano shupavu na mashujaa wa Palestina hatimaye itamaliza na kuyakatisha maisha ya aibu ya wavamizi wa Palestina."
-
Onyo Kali la Iran kwa Marekani na Utawala wa Kizayuni
Apr 03, 2025 09:08Katika mazingira ya kuongezeka kwa vita vya kisaikolojia vinavyoendeshwa na Marekani pamoja na utawala wa Kizayuni, na vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa Donald Trump na maafisa waandamizi wa usalama wa utawala wake huko Washington kuhusu uwezekano wa kushambulia Iran iwapo kutakosekana makubaliano kuhusu suala la nyuklia, Tehran imetoa onyo kali kwa Marekani na Israel kuhusu madhara makubwa ya hatua yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran.