-
Araqchi: Wanaotoa silaha kwa Israel wanaishutumu Iran kutuma makombora huko Russia
Nov 20, 2024 04:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Umoja wa Ulaya na Uingereza zinatumia mienendo inayokinzana dhidi ya Iran ambayo inafichua sera za undumakuwili na kukwepa wajibu wao wa kulinda haki za binadamu.
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Gaza imekuwa kaburi la watoto
Nov 20, 2024 04:38Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, Ukanda wa Gaza umegeuka kuwa kaburi la watoto kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala unaofanya mauaji ya kimbari wa Israel.
-
Araqchi: Ipo nia ya dhati ya kupanua ushirikiano na Syria katika nyanja zote
Nov 19, 2024 23:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina nia ya dhati ya kupanua ushirikiano kati yake na Syria katika nyanja jzote.
-
Kolivand: Iran kutuma tani 10 za misaada kwa watu wa Lebanon
Nov 19, 2024 23:08Mkuu wa Shirika la Hilali Nyekundu la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRCS) ameeleza kuwa shirika hilo hivi karibuni litatuma tani 10 za misaada mbalimbali iliyotolewa na wananchi wa Iran kwa ajili ya wenzao wa Lebanon.
-
Kuendelea vitendo vya uhasama vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Iran
Nov 19, 2024 10:07Katika kuendeleza hatua zake za kiuadui dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Jumatatu ya jana tarehe 18 Novemba Umoja wa Ulaya ulitoa taarifa na kuliwekea vikwazo Shirika la Meli la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa kampuni hiyo kwa kisingizio na madai yasiyo na msingi ya eti Iran kuingilia mzozo wa Ukraine.
-
Kiongozi Muadhamu: Tutaendelea kuwa pamoja na wananchi wa Lebanon na Muqawama
Nov 19, 2024 07:43Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe wa maneno kwa ajili ya wananchi na viongozi wa Lebanon walioko kwenye vita hivi sasa na kuwaambia kuwa, sisi hatuna tofauti na nyinyi, tuko pamoja nanyi na tutaendelea kuwa pamoja nanyi.
-
Araghchi: Iran itatoa majibu kwa Israel katika wakati itakaoona unafaa
Nov 19, 2024 07:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia jinai ya Israel ya kushambulia ardhi ya Iran na kusema kuwa Jamhuri ya Kiislamu itatoa majibu kwa utawala wa Kizayuni katika muda inaoona unafaa na kwamba Tehran bado inahifadhi haki yake ya kutoa majibu makali kwa Israel.
-
Wakuu wa IRIB watoa salamu za rambirambi baada ya kuuawa shahidi msemaji wa Hizbullah
Nov 19, 2024 03:21Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB), Peyman Jebelli, na Mkuu wa Kitengo cha Kimataifa cha IRIB, Ahmad Noroozi wametoa taarifa tofauti wakituma salamu za rambi rambi kufuatia kuuawa shahidi msemaji wa Hizbullah ya Lebanon katika hujuma ya kigaidi ya Israel.
-
Balozi mpya wa Kenya akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
Nov 19, 2024 03:11Balozi mpya wa Kenya nchini Iran amekutana na Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kumkabidhi nakala za hati zake za utambulisho.
-
Mhandisi Muirani ajiuzulu Google kulamikia ushirikiano wa kampuni hiyo na Israel katika mauaji ya kimbari Gaza
Nov 19, 2024 03:01Mhandisi wa program za kompyuta wa Iran, Alireza Zakeri ametangaza kujiuzulu kutoka shirika la Google kutokana na ushirikiano wa kampuni hiyo kubwa ya kiteknolojia ya Marekani na utawala katili wa Israel katika mauaji ya kimbari ya utawala huyo dhidi ya Wapalestina wa Gaza.