Upinzani Kenya: Maafisa wa uchaguzi wametishiwa maisha
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i34077-upinzani_kenya_maafisa_wa_uchaguzi_wametishiwa_maisha
Kiongozi wa Muungano wa upinzani Kenya (NASA) Raila Odinga amesema leo kuwa maisha ya baadhi ya maafisa wa ngazi ya juu wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo yanakabiliwa na tishio kubwa kutoka serikalini kabla ya kufanyika uchaguzi mpya wa rais mwezi ujao.
(last modified 2026-02-25T03:34:48+00:00 )
Sep 08, 2017 12:31 UTC
  • Upinzani Kenya: Maafisa wa uchaguzi wametishiwa maisha

Kiongozi wa Muungano wa upinzani Kenya (NASA) Raila Odinga amesema leo kuwa maisha ya baadhi ya maafisa wa ngazi ya juu wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya nchi hiyo yanakabiliwa na tishio kubwa kutoka serikalini kabla ya kufanyika uchaguzi mpya wa rais mwezi ujao.

Odinga ambaye amefanikiwa kuzuia ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta mahakamani, amewaambia waandishi wa habari kuwa baadhi ya maafisa wa tume hiyo ya uchaguzi wamepokea baruapepe zinazotishia masiaha yao na kwamba wameondolewa ulinzi.

Odinga amesema kuwa kwa sasa wapinzani wanakabiliwa na hatari kubwa na amemtaka rais Uhuru Kenyatta ajiuzulu. Serikali ya Kenya kwa upande wake haijatoa maelezo yoyote kuhusu madai hayo ya Odinga.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya 

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya inakabiliwa na mashinikizo ya wapinzani wanaoitaka ifanye marekebisho baada ya Mahakama ya Juu ya nchi hiyo kutengua ushindi wa Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa rais wa mwezi uliopita wakisema kuwa kulikuwa na kasoro katika uchaguzi huo.