Evariste Ndayishimiye rais mpya wa Burundi + Sauti
May 26, 2020 02:20 UTC
Tume ya uchaguzi ya Burundi, jana Jumapili ilimtangaza Evariste Ndayishimie kuwa rais mpya wa nchi hiyo huku ishara zote zikiwa zimeonesha tangu awali kabisa kwamba mgombea huyo wa chama tawala angelitangazwa mshindi katika uchaguzi wa rais.
Vyombo vya habari viliashiria kuwa, Ndayishimiye ambaye ni jenerali wa kijeshi kutoka chama tawala cha CNDD-FDD ndiye mtarajiwa mkuu wa kurithi kiti cha Rais Pierre Nkurunziza. Agathon Rwasa, mgombea mkuu wa upinzani amelalamikia matokeo hayo na kusema kumefanyika udanganyifu mkubwa.
Tags