Chama kilichoondolewa madarakani Burkina Faso chataka Kabore aachiwe huru
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i80722-chama_kilichoondolewa_madarakani_burkina_faso_chataka_kabore_aachiwe_huru
Chama cha Rais aliyepinduliwa nchini Burkina Faso, Roch Marc Christian Kabore, kimekita kikosi cha wafanya mapinduzi kilichotwaa madaraka kimwachie huru bila ya masharti yoyote rais huyo wa zamani wa Burkina Faso ambaye yuko katika kifungo cha nyumbani.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Feb 24, 2022 10:42 UTC
  • Chama kilichoondolewa madarakani Burkina Faso chataka Kabore aachiwe huru

Chama cha Rais aliyepinduliwa nchini Burkina Faso, Roch Marc Christian Kabore, kimekita kikosi cha wafanya mapinduzi kilichotwaa madaraka kimwachie huru bila ya masharti yoyote rais huyo wa zamani wa Burkina Faso ambaye yuko katika kifungo cha nyumbani.

Chama hicho kilichoondolewa madarakani nchini Burkina Faso kimetoa wito huo ikiwa umepita mwezi mmoja tangu Christian Kabore atiwe nguvuni na wanajeshi  Januari 24 mwaka huu katika mji mkuu Ouagadougou. 

Mwenyekiti wa chama hicho Allasane bala Sakande amesema kuwa Chama cha Maendeleo ya Wananchi kina wasiwasi na kinahoji sababu za kuendelea kushikiliwa nyumbani Christian Kabore. Chama  hicho pia kimemtaka mkuu wa kikosi cha wanajeshi waliofanya mapinduzi, Luteni Kanali Paul-Henri Sandaogo Damiba, kutekeleza ahadi alizotoa kwamba atahakikisha haki za msingi za kila raia zinalindwa. 

Paul-Henri Sandaogo Damiba kiongozi wa wafanya mapinduzi Burkina Faso

Kabore alikamatwa na kuwekwa chini ya kifungo cha nyumbani katika wilaya ya Ouaga 2000 baada tu ya mapinduzi ya jeshi la Burkina Faso.

Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika (Ecowas) zimetoa wito wa kuachiwa huru rais huyo wa zamani wa Burkina Faso.