Magaidi zaidi 100 wa Al-Shabaab waangamizwa Somalia
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i89694-magaidi_zaidi_100_wa_al_shabaab_waangamizwa_somalia
Serikali ya Somalia imetangaza kuwa magaidi zaidi ya 100 wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Al-Shabaab wameangamizwa kusini mwa nchi hiyo.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Oct 26, 2022 02:32 UTC
  • Magaidi zaidi 100 wa Al-Shabaab waangamizwa Somalia

Serikali ya Somalia imetangaza kuwa magaidi zaidi ya 100 wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Al-Shabaab wameangamizwa kusini mwa nchi hiyo.

Al-Shabaab ni kundi la kigaidi la wabeba silaha lenye mafungamano na mtandao wa Al-Qaeda na limepanga na kutekeleza operesheni nyingi za kigaidi ambazo zimeua mamia ya watu barani Afrika.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Fars, serikali ya Somalia imetangaza kuwa zaidi ya wanamgambo mia moja wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameuawa katika operesheni zilizotekelezwa na jeshi la nchi hiyo katika siku chache zilizopita kwenye eneo la Shabelle ya Kati kusini mwa nchi hiyo.
 
Kabla ya hapo, jeshi la Somalia lilitangaza siku ya Jumapili Oktoba 9, kwamba wanamgambo 200 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab waliuawa katika eneo la Hiran katika operesheni ya vikosi vya jeshi la nchi hiyo.

Kundi la kigaidi la al-Shabaab limeshambulia mara kwa mara wanajeshi wa serikali na wa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia, na limehusika pia na operesheni kadhaa za umwagaji damu katika maeneo mengine ya Afrika.

Kundi hilo la ukufurishaji limekuwa likijaribu kuipindua serikali kuu ya Somalia tangu mwaka 2007.

Al-Shabaab walifukuzwa Mogadishu na Jeshi la Somalia na vikosi vya Umoja wa Afrika mwaka 2011; hata hivyo, kundi hilo la kigaidi lingali linadhibiti maeneo mengi ya vijijini katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.../