-
Wasiwasi wa Marekani kuhusu muungano wa Iran, Russia na China
Mar 23, 2024 22:56Kamanda wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) Jenerali Michael E. Kurilla amebainisha wasiwasi wake kuhusu kuongezeka kwa ushirikiano kati ya Iran, China na Russia na kudai kuwa ushirikiano wa nchi hizo utakuwa na"matokeo mabaya ya kimataifa".
-
Kula mweleka njama za Marekani za kuunga mkono mauaji ya kimbari ya Israel kwenye UN
Mar 23, 2024 08:11Azimio lililopendekezwa na Marekani la kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza limegonga ukuta baada ya kupigiwa kura ya veto na Russia na China ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Wito wa maseneta 19 wa Marekani wa kuundwa taifa huru la Palestina
Mar 22, 2024 22:59Maseneta 19 wa chama cha Democratic wametoa wito wa kuundwa taifa huru la Palestina katika barua yao iliyotumwa kwa Rais wa Marekani, Joe Biden.
-
Uchambuzi wa vita vya Gaza katika hotuba ya Nowruz ya kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Mar 22, 2024 03:34Katika hotuba yake ya siku ya kwanza ya mwaka mpya wa 1403 Hijria Shamsia, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amesema suala la Palestina na Gaza ni suala la daraja ya kwanza la kimataifa na kusisitiza kuwa: Kadhia ya Gaza imeonesha jinsi ulimwengu eti uliostaarabika na unaodai kutetea haki za binadamu, unavyofanya dhulma kubwa dhidi ya watu wa Gaza.
-
Kuendelea mapambano, mhimili wa muqawama dhidi ya mauaji ya kimbari ya Gaza
Mar 21, 2024 22:54Ikiwa ni katika kukabiliana na muendelezo wa mashambulizi ya kinyama ya Israel katika Ukanda wa Gaza, mhimili wa muqawama wa Palestina, Lebanon, Iraq na Yemen umeshambulia maeneo kadhaa ya Wazayuni.
-
Ukosoaji wa Afrika Kusini dhidi ya Israel kwa kukaidi uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Mar 21, 2024 04:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini amesema kuwa kutotekelezwa maamuzi ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki dhidi ya Israel kunaidhoofisha mahakama hiyo.
-
Maadhimisho ya kupitishwa kwa sheria ya kutaifishwa kwa sekta ya mafuta ya Iran
Mar 20, 2024 04:28Siku ya mwisho katika kalenda ya Hijria Shamsia ya Iran ambayo ilikuwa jana ni maarufu kama "Siku ya Kutaifisha Sekta ya Mafuta". Katika siku hii, miaka 73 iliyopita baada ya vuta nikuvute na mapambano ya wananchi wa Iran dhidi ya mkoloni Mwingereza na utawala kibaraka wa mfalme hapa nchini, hatimaye wabunge wa Bunge la Taifa walipitisha muswada wa kutaifisha sekta ya mafuta nchini.
-
Hatua ya serikali ya Niger ya kufuta makubaliano ya kijeshi na Marekani
Mar 19, 2024 23:06Amadou Abdurrahman, Msemaji wa Serikali ya Niger, ametangaza kupitia taarifa kwamba nchi hiyo imefuta makubaliano yote ya kijeshi na Marekani ambayo yaliruhusu nchi hiyo ya Magharibi kuweka majeshi yake katika ardhi ya Niger.
-
Ushindi mkubwa wa Putin katika uchaguzi wa rais wa Russia
Mar 19, 2024 02:42Tume Kuu ya Uchaguzi ya Shirikisho la Russia imetangaza kuwa Vladimir Putin, rais wa sasa wa nchi hiyo, ameshinda uchaguzi wa karibuni kwa asilimia 87.32 ya kura na hivyo kupata fursa nyingine ya kuwa rais wa Russia kwa muhula mwingine wa miaka sita. Kwa mujibu wa tangazo la tume hiyo, kiwango cha ushiriki katika uchaguzi kilikuwa cha zaidi ya asilimia 70.
-
Kuwekwa vikwazo vipya dhidi ya Iran
Mar 18, 2024 23:09Wizara ya Fedha ya Marekani kwa mara nyingine imeamua kuweka vikwazo vipya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.