-
Uamuzi wa Russia na Qatar wa kutumia sarafu zao za taifa katika miamala ya kibiashara
Aug 10, 2023 22:47Katika muendelezo wa sera ya kufuta sarafu ya dola katika miamala ya kibiashara kati ya nchi mbalimbali, Qatar pia imeondoa matumizi ya dola katika mabadilishano yake ya kibiashara na Russia, ambapo biashara baina ya nchi hizo mbili, sasa itafanyika kwa kutumia sarafu za taifa.
-
Uwezo wa nguvu na amani ya Iran ilivyopatikana kwa ujasiri na ushujaa wa Walinzi wa Haram
Aug 10, 2023 06:03Rais Ebrahim Raisi ameashiria kuainishwa katika kalenda rasmi ya Iran tarehe 18 Mordad, inayosadifiana na Agosti 9, kuwa Siku ya Mashahidi Walinzi wa Haram na akaienzi kumbukumbu ya Mashahidi hao kwa kusema: Mashahidi Walinzi wa Haram ni walinzi wa heshima na utakatifu wa Uislamu, ambao walitetea thamani za dini kwa roho zao na kufa shahidi katika njia hiyo.
-
Ombi rasmi lililowasilishwa na nchi 23 la kujiunga na jumuiya ya BRICS
Aug 09, 2023 22:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Naledi Pandor ametangaza kuwa viongozi wa nchi 23 wameeleza rasmi nia ya nchi zao kujiunga na jumuiya ya BRICS. Mwanadiplomasia huyo amesema: "tumepokea taarifa rasmi za viongozi wa nchi 23 wanaotaka nchi zao kujiunga na BRICS, na tuna maombi yasiyo rasmi pia ya nchi zenye uwezekano wa kujiunga na BRICS".
-
Kuimarishwa uwepo wa kijeshi wa Marekani katika Ghuba ya Uajemi na matokeo yake
Aug 09, 2023 03:51Kuimarishwa uwepo wa kijeshi wa Marekani katika Ghuba ya Uajemi ni miongoni mwa maudhui zinazopewa uzito siku hizi na kufuatiliwa kwa karibu na vyombo vya habari; na kwa kutilia maanani uhitaji ilionao Marekani na utawala wa Kizayuni kwa jambo hilo, habari zinazohusiana na harakati mpya za kijeshi zilizoanzishwa na Washington katika eneo hili zinaakisiwa kwa upana na uzito mkubwa zaidi na vyombo vya habari vya Magharibi na vya Kizayuni.
-
Kukosoa Maduro kimya cha viongozi wa Ulaya kuhusu kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu
Aug 08, 2023 23:41Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amekosoa vikali kuendelea kukaa kimya viongozi wa Ulaya kuhusiana na kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu.
-
Kushadidi wahaka wa shakhsia wa kiusalama kuhusu kufikia mwisho uhai wa utawala wa Kizayuni wa Israel
Aug 08, 2023 04:54Tamir Pardo, mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel (Mossad) ametangaza kuwa, utawala huo unakaribia mwisho wake.
-
Wasiwasi wa Baraza la Usalama kwa hali ya kibinadamu nchini Afghanistan
Aug 07, 2023 22:38Akthari ya washiriki katika mkutano wa hivi karibuni wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa chini ya kichwa "Ukosefu wa Usalama wa Chakula Duniani" walionyesha wasiwasi walionao kwa hali ya kibinadamu nchini Afghanistan.
-
Changamoto ya nishati na vita vya kuwania madaraka nchini Niger
Aug 07, 2023 09:29Licha ya kumalizika muda uliowekwa na ECOWAS kwa baraza la kijeshi la Niger kuhusu kukabidhi madaraka, lakini hakuna ishara zozote zinazoonesha kuwa jumuiya hiyo ya kiuchumi ya magharibi mwa Afrika iko tayari kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya wanajeshi waliofanya mapinduzi nchini humo.
-
Utawala wa Netanyahu umechochea mapingano katika kambi ya Wapalestina ya Ain Halweh
Aug 06, 2023 23:09Kwa bahati nzuri, usitishaji mapigano upo katika kambi ya wakimbizi ya Kipalestina huko Ain Al-Hilweh, iliyoko kusini mwa Lebanon, na juhudi za kisiasa, haswa za vikundi vya muqawama wa Lebanon na Palestina, zinaendelea ili kudumisha usitishaji mapigano.
-
Miaka mitatu baada ya mlipuko wa Beirut bado kesi ya kadhia hii haijatatuliwa
Aug 06, 2023 07:01Ikiwa imetimia miaka mitatu tokea kujiri mlipuko wa kutisha huko Beirut mchakato wa mahakama katika kesi ya mlipuko huo bado haujakamilika na Lebanon bado inatawaliwa na serikali ya mpito.