-
Mchezo mpya wa kuigiza wa serikali wa Biden wa kujisafisha na chuki dhidi ya Uislamu
Dec 23, 2024 23:09Wakati Marekani inaendelea kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Israel huko Gaza, serikali ya Joe Biden imeidhinisha kimaonyesho tu hati ya "Kupambana na Chuki dhidi ya Uislamu" ili kujitakasa bila kutaja mizizi na chanzo cha ukatili na chuki hizo za serikali dhidi ya Waislamu nchini Marekani.
-
Ugaidi, chombo cha kisiasa cha nchi za Magharibi
Dec 23, 2024 10:14Licha ya kupita siku kadhaa tangu tukio la watu kugongwa na gari katika soko la Krismasi la Magdeburg, Ujerumani, suala hili bado linagonga vichwa vya habari katika vyombo vya habari vya Magharibi. Makumi ya watu waliuawa auu kujeruhiwa katika tukio hilo.
-
Stratejia za busara na athirifu za Iran katika kuihami kambi ya muqawama
Dec 22, 2024 23:39Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameweka wazi misimamo ya Jamhuri ya Kislamu ya Iran kuhusu matukio ya kikanda na kimataifa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza hayo katika mahijiano maalumu aliyofanya na mtandao wa Misri wa al Ghad pambizoni mwa mkutano wa wakuu wa nchi za Kiislamu zinazoendelea yaani D-8 mjini Cairo, Misri.
-
Rais wa Ufaransa akiri, Afrika imebadilika
Dec 22, 2024 08:48Wakati Ufaransa imepoteza kambi zake nyingi za kijeshi barani Afrika, sasa rais wa nchi hiyo, Emmanuel Macron, katika safari ya kimyakimya kwenye kituo cha mwisho cha operesheni za nchi hiyo huko Djibouti, amekiri kwamba: Afrika inabadilika kwa sababu maoni ya umma na Serikali yamo katika hali ya kubadilika, hivyo nafasi yetu barani Afrika pia itabadilika.
-
Wimbi kubwa la kujiuzulu maafisa wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel
Dec 22, 2024 00:53Duru za Kiebrania zimeripoti kuwa mamia ya maafisa wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamejiuzulu kutokana na kuendela vita vya utawala huo dhidi ya watu wa Gaza, vinavyoendelea kuutafuna kwa ndani utawala huo.
-
Mapendekezo matano ya Iran katika mkutano wa D8
Dec 21, 2024 09:15Mapendekezo matano yaliyototolewa na Iran kuhusu nafasi na wajibu wa kundi la "D8" kuhusu Gaza yanaonyesha kuwa, sambamba na matukio ya hivi sasa ya Syria, kuna ulazima wa kuwepo umoja na mshikamano zaidi na zaidi wa nchi za Kiislamu katika kipindi cha sasa, kuliko wakati mwingine wowote, hususan kuhusu masuala ya Palestina.
-
Haki za binadamu; wenzo wa kisiasa wa madola ya Magharibi
Dec 20, 2024 23:22Canada, kama ilivyokuwa katika miaka ya hivi karibuni, imewasilisha kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa rasimu ya azimio kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu nchini Iran na kupasishwa kwa mbinde katika kamati ya tatu ya Baraza Kuu.
-
Mauaji ya kimbari ya Wazayuni dhidi ya vyombo vya habari Ukanda wa Gaza
Dec 19, 2024 23:14Kamati ya Kuwalinda Waandishi wa Habari ya Palestina (CPJ) imeashiria katika taarifa yake kuhusu jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wanahabari na kuitolea wito jamii ya kimataifa kuuwajibisha utawala huo kutokana na jinai zake huko Gaza.
-
D8, nembo ya nguvu ya Ulimwengu wa Kiislamu
Dec 19, 2024 06:16Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, yuko Misri anakoshiriki mkutano wa 11 wa viongozi wa nchi za kundi la D8.
-
Marekani na Ujerumani, washirika wa mauaji ya kimbari yanayofanywa na Wazayuni Gaza
Dec 18, 2024 23:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ameashiria sehemu ya maelezo yaliyotolewa na Ben Saul, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa, kwamba Ujerumani na Marekani zinachangia asilimia 99 ya silaha inazopatiwa Israel na akabainisha kwamba nchi hizo mbili ni washirika wa mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.