-
ACT-Wazalendo yalalamika kufanyiwa hujuma visiwani Zanzibar + Sauti
Dec 02, 2019 13:31Viongozi wa chama cha ACT Wazalendo visiwani Zanzibar wametahadharisha kuhusu madhara yanayoweza kutokea kutokana na kile wanachoamini ni hujuma za makusudi zinazoendeshwa dhidi ya viongozi wa chama hicho visiwani Unguja na Pemba. Harith Subeit na maelezo zaidi kutoka Zanzibar.
-
Tume ya Uchaguzi Uganda yakumbwa na kashfa nyingine mpya + Sauti
Dec 02, 2019 13:29Baada ya Tume ya Uchaguzi nchini Uganda kufunguliwa mashtaka ya makosa ya kukaa ofisini kinyume cha sheria, tume hiyo sasa imekumbwa na kashfa nyingine ya kisiasa... Kigozi Ismail na maelezo zaidi kutoka Kampala.
-
SAUTI, Wafanyabiashara wa jiji la Bujumbura waitaka serikali iwaonee huruma kutokana na amri ya meya wa mji huo
Nov 28, 2019 13:13Baada ya Meya wa jiji la Bujumbura Freddy Mbonimpa, kutangaza operesheni ya hatua 10 alizozitaja kama njia yenye lengo la kuinuwa uchumi na kuimarisha usalama mjini hapo, tayari polisia imeanzisha msako wa kuwakamata machinga wanaojishughulisha katika maeneo ambayo hayajaratibiwa kufanyia shughuli hizo.
-
SAUTI, Wafuasi wa kiongozi wa waasi nchini CAR waijia juu serikali wakiitaka isimpandishe kizimbani bosi wao
Nov 28, 2019 13:13Wafuasi wa Abdullah Miskin, Kiongozi wa moja ya makundi mashuhuri nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wameijia juu serikali ya Bangui wakiitaka kutomrejesha nchini humo kiongozi wao huo akiwa chini ya ulinzi.
-
SAUTI, Mfumo wa Taifa wa Bima ya Afya Tanzania waja na mpango wa kifurushi uliokosolewa na wanasiasa
Nov 28, 2019 13:04Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini Tanzania (NHIF) umekuja na njia ambayo imetajwa kuwa ni suluhisho la wananchi wengi wenye hali ngumu kukosa huduma hiyo.
-
Viongozi wa Kenya wazindua ripoti ya BBI + Sauti
Nov 28, 2019 03:32Viongozi nchini Kenya wamezindua ripoti ya uwiano na utangamano wa kisiasa huku wakifanya juhudi za kuleta muamko mpya wa kisiasa na mshikamano katika kila fani ya maisha nchini humo. Seifullah Murtadha na maelezo zaidi kutoka Mombasa...
-
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi atembelea eneo aliloshambuliwa na waasi + Sauti
Nov 25, 2019 12:34Wiki moja baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha walotajwa na jeshi la Burundi kwamba walitokea katika nchi jirani ya Rwanda, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi, Pascal Barandagiye, ametembelea tarafa ya Mabayi na kuwataka raia na watawala kuwa makini juu ya suala la usalama wakati huu ambapo imebakia miezi 6 tu kabla ya kufanyika uchaguzi nchini Burundi. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura.
-
Zaidi ya familia 50 zahamishwa katika mpaka wa Uganda na Kenya kutokana na mafuriko + Sauti
Nov 25, 2019 12:10Familia zaidi ya 50 zimehamishwa kutoka kwenye mpaka wa Uganda na Kenya kutokana na kuhofia maafa yanayoweza kusababishwa na mvua kubwa zinazonyesha mfululizo. Kigozi Ismail na ripoti zaidi kutoka Kampala.
-
Idadi ya waliofariki dunia kwenye ajali ya ndege DRC yaongezeka + Sauti
Nov 25, 2019 12:06Idadi ya watu waliofariki dunia baada ya kuanguka ndege ndogo ya abiria katika mji wa Goma wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeongezeka na kufikia watu 29 wakiwemo watu tisa wa familia moja. Watu wengine 19 wamejeruhiwa. Ndege hiyo iliyokuwa inaelekea Beni kutokea Goma ilianguka juu ya nyumba ya watu na kuua watu waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo. Mossi Mwassi na maelezo zaidi
-
SAUTI, Mkasa wa kusikitisha kuhusiana na tukio la maporomoko ya ardhi na mafuriko nchini Kenya
Nov 25, 2019 07:40Viongozi wa serikali ya Kenya wametangaza habari ya kuongezeka idadi ya wahanga wa mafuriko na maporomoko ya ardhi kuwa imefikia watu 60.