Nov 10, 2023 07:21 UTC
  • Kanani: Watoto wa Palestina daima wamekuwa ni jinamizi kwa Wazayuni

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mjibizo kwa shambulio lililofanywa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya Hospitali ya Watoto ya Al-Nasr huko Gaza, na kueleza kwamba: "watoto wa Kipalestina daima wamekuwa ni jinamizi kwa Wazayuni."

Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim, Nasser Kanani amelaani shambulio la kinyama la utawala wa Kizayuni dhidi ya Hospitali ya Watoto ya Al-Nasr katika Ukanda wa Gaza na kusema: watoto wa Kipalestina wanajifunza alfabeti za maneno ya subira, ushujaa, muqawama na kuuawa shahidi kwa ajili ya ukombozi wa Palestina kuanzia siku za mwanzo za kuzaliwa kwao katika madrasa za mama zao, baba na kaka zao na dada zao na hilo ndilo jinamizi la kudumu linalowaandama Wazayuni.
 
Kanani amesisitiza kuwa: Wazayuni wanadhani kwamba ikiwa watawachinja watoto wote wa Gaza, watakuwa wameshawafuta tokea leo kwenye mbeleko za mama zao wapiganaji na wanajihadi wa kesho wa Palestina, ilhali kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, mama wa Kipalestina atamkabidhi kwa mara nyingine mtoto wake kwa mkondo wa maji ili muda si mrefu wa kesho ijayo aje kuuanganmiza utawala usio na mashiko wa Mafirauni wa Kizayuni.
Nasser Kanani

Katika jibu ililotoa kwa madhila ya zaidi ya miongo saba ya kukaliwa kwa mabavu Palestina na zaidi ya miaka kumi na tano ya kuwekewa mzingiro Gaza na kufungwa jela na kuteswa maelfu ya Wapalestina, mnamo tarehe 7 Oktoba, Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) ilianzisha operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.

Operesheni hiyo inachukuliwa kuwa moja ya mashambulio makali zaidi dhidi ya utawala dhalimu wa Kizayuni. Wapiganaji wa Hamas walipenya kwenye maeneo yanayokaliwa kwa mabavu kupitia nukta kadhaa za uzio wa mpakani na kushambulia vijiji kadhaa, ambapo mbali na kuangamiza idadi kubwa ya Wazayuni, waliwakamata mateka wengine kadhaa miongoni mwao.

Ili kufidia kushindwa kwake katika operesheni za Muqawama, tokea Oktoba 7 hadi sasa utawala wa Kizayuni umekuwa ukifanya mashambulio ya kinyama na ya mtawalia dhidi ya maeneo tofauti ya Ukanda wa Gaza; na matokeo yake Wapalestina zaidi ya elfu kumi wameshauawa shahidi hadi sasa na wengine wasiopungua elfu 27 wamejeruhiwa.../

 

Tags