Iran yalaani mashambulizi ya anga ya Uturuki katika ardhi ya Iraq
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i28302-iran_yalaani_mashambulizi_ya_anga_ya_uturuki_katika_ardhi_ya_iraq
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mashambulizi ya anga ya Uturuki huko Iraq na kuyataja kuwa ni ukiukaji wa mamlaka ya kitaifa na umoja wa ardhi ya Iraq.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Apr 26, 2017 23:20 UTC
  • Iran yalaani mashambulizi ya anga ya Uturuki katika ardhi ya Iraq

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mashambulizi ya anga ya Uturuki huko Iraq na kuyataja kuwa ni ukiukaji wa mamlaka ya kitaifa na umoja wa ardhi ya Iraq.

Ndege za kivita za Uturuki Jumanne alfajiri ziliyashambulia baadhi ya maeneo ya mji wa Sinjar mkoani Nainava kwa kisingizio cha kuwepo ngome za wapiganaji wa chama cha Kikurdi cha PKK. Watu kadhaa waliuawa katika mashambulizi hayo ya Uturuki. 

Makao makuu ya kikosi cha ulinzi cha Wakurdi yaliyoshambuliwa na Uturuki 

Bahram Qassemi Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameunga mkono msimamo wa serikali ya Iraq katika uwanja huo ikiwa ni radiamali yake kwa mashambulizi hayo ya anga ya Uturuki katika maeneo ya kandokando mwa mji wa Sinjar huko Iraq. Qassemi amesisitiza pia kuwa kukiuka mamlaka ya kitaifa ya nchi nyinginezo kwa lengo na uhalalishaji wowote ule, ni sawa na kukiuka sheria za kimataifa. Amesema jambo hilo linaweza kuandaa uwanja wa kushtadi machafuko katika eneo la Mashariki ya Kati.