-
Iran yamuonya mkuu wa IAEA: Vitisho vilivyofeli havitaleta isipokuwa kusindwa kwingine
Oct 24, 2025 00:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amemuonya mkuu wa shirika la nyuklia la Umoja wa Mataifa, Rafael Grossi, dhidi ya kutoa "vitisho vilivyoshindwa" dhidi ya Tehran, akisema matamshi kama hayo hayataleta "isipokuwa kushindwa kwingine."
-
Mahdieh Esfandiari Muirani mtetezi wa Palestina aachiliwa huru
Oct 23, 2025 23:24Mahdieh Esfandiari, mwanaharakati wa Iran anayewaunga mkono watu wa Palestina, ameachiliwa kwa masharti kutoka katika jela ya Ufaransa baada ya kuzuiliwa kwa zaidi ya miezi saba.
-
Waziri wa Usalama wa Taifa: Iran haina imani kuhusu kulindwa maslahi ya taifa kupitia mazungumzo na Marekani
Oct 23, 2025 07:47Waziri wa Usalama wa Taifa wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu haina imani kabisa kuhusu kulindwa maslahi ya nchi hii kupitia kufanya mazungumzo na Marekani.
-
Iran: Mashirika 50 ya kijasusi yaliisaidia Israel katika Vita vya Siku 12 dhidi yetu
Oct 22, 2025 23:41Waziri wa Usalama wa Taifa wa Iran amesema: Katika vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel mwezi Juni mwaka huu dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, adui alipanga kuzusha uvunjifu mkubwa wa amani nchini Iran na alijaribu kutumia magaidi wake wote wakufurushiaji walioachiwa huru huko Syria na Afghanistan kwa ajili ya kuvuruga usalama wa Iran ya Kiislamu lakini alishindwa. Mashirika 50 ya kijasusi yaliisaidia Israel lakini pia yalishindwa.
-
Iran: Hatutarudi kwenye meza ya mazungumzo hadi Marekani iachane na sera zake za kupenda makuu
Oct 22, 2025 23:11Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, sharti la kurejea Iran katika meza ya mazungumzo ni Wamarekani kuacha siasa zao za kijuba na za kupenda makuu.
-
Larijani aishukuru Russia kwa kuiunga mkono Tehran katika Baraza la Usalama
Oct 22, 2025 09:34Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amewasilisha kwa Russia shukrani za Jamhuri ya Kiislamu kutokana na hatua ya Moscow ya kuunga mkono msimamo wa haki za Tehran katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mkabala wa hatua ya nchi za Magharibi ya kurejeshea hatua kali za kiuchumi dhidii ya Iran.
-
Iran yaidhinisha rasmi kujiunga na mkataba wa kupambana na ufadhili wa ugaidi
Oct 22, 2025 09:23Rais Masoud Pezeshkian amewasilisha rasmi sheria ya kujiunga Iran na Mkataba wa Kimataifa wa Kupambanana Ufadhili wa Ugaidi (CFT).
-
Iran yagundua maficho ya televisheni ya Israel inayoeneza uadui dhidi yake
Oct 22, 2025 02:47Operesheni ya kiintelijensia ya Iran iliyofanyika kwa mafanikio, imefichua waliko watu wanaohusika na shirika la kijasusi la Israel Mossad, ambao waliwatumikia maadui hasa Israel na Marekani wakati wa vita vya upashaji habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu Iran.
-
Larijani: Marekani haitaki Iraq iwe huru/ Baghdad: Usalama wetu na wa Iran ni kitu kimoja
Oct 22, 2025 02:46Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema: Ni lazima tufanye juhudi za kuzuia njama zozote zinazofanywa na watu baki wenye nia mbaya ya kuyaletea madhara mataifa ya Iran na Iraq.
-
Meja Jenerali Pakpour: Jahanamu itashuhdiwa iwapo Iran itashambuliwa
Oct 21, 2025 23:48Iran iko tayari kutoa jibu kali kwa uchokozi wowote endapo utafanywa dhidi yake katika siku zijazo. Ameyasema hayo Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ambaye ametaharisha kuwa Iran "itaachilia moto wa kuzimu dhidi ya adui."