-
Afisa mwandamizi wa usalama wa Iran akutana na Putin, ampa ujumbe wa Kiongozi Muadhamu
Oct 17, 2025 03:58Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Larijani amekutana na Rais Vladimir Putin wa Russia mjini Moscow, na kumkabidhi ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
-
Unyanyuaji Uzani; Muirani avunja rekodi ya dunia, ashinda dhahabu Misri
Oct 17, 2025 03:20Ali Akbar Gharibshahi, bingwa wa mchezo wa kunyanyua vitu vizito wa Iran ameweka rekodi mpya ya dunia na kushinda medali ya dhahabu katika kategoria ya kilo wanamichezo wenye 107, kwenye Mashindano ya Dunia ya Kunyanyua Uzani ya 2025 nchini Misri.
-
Pezeshkian: Vijana wa Iran wamebobea katika uzalishaji wa makombora
Oct 16, 2025 23:12Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria uwezo wa kustaajabisha wa vijana wa Jamhuri ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, vijana wa taifa hili ndio ambao wanatengeneza makombora na nishati ya nyuklia kwa kutegemea uwezo wao.
-
Mawaziri wa Iran na Tunisia: Utatuzi wa kadhia ya Palestina ni kukomeshwa uvamizi wa Israel
Oct 16, 2025 22:46Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Tunisia wamesisitiza kuwa, kulitatua suala la Palestina kunahitaji kukomeshwa kukaliwa kwa mabavu na kutekelezwa haki ya kujitawala wananchi wa Palestina.
-
Araqchi asisitiza kupanuliwa uhusiano wa Iran na Uganda katika nyanja za kiuchumi na kilimo
Oct 16, 2025 09:08Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran iko tayari kupanua uhusiano na Uganda katika nyanja za kiuchumi, kilimo na biashara.
-
Kuihami Palestina na kuimarisha ushirikiano wa pande kadhaa; Msimamo wa Iran katika Mkutano wa NAM
Oct 16, 2025 07:21Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mambao ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Kampala, mji mkuu wa Uganda kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wanachama wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM).
-
Araqchi: Nchi wanachama wa NAM zinapinga utaratibu wa "Snapback"
Oct 16, 2025 06:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuhusu taarifa ya mwisho ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) kwamba: "Kwa mtazamo wa jumuiya hiyo, Azimio nambari 2231 la Umoja wa Mataifa bado ni halali na vipenege na muda wa azimio hilo vinapaswa kuzingatiwa.
-
Kharrazi: Iran iko tayari kwa mazungumzo, lakini haitakubali kuburuzwa
Oct 16, 2025 06:12Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Mahusiano ya Kigeni ya Iran, Kamal Kharrazi amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kwa mazungumzo, lakini katu haitakubali kutwishwa matakwa ya aina yoyote.
-
Kamanda Asadi: Kusitisha mapigano Ghaza kunatokana na kukata tamaa Marekani na Israel
Oct 16, 2025 02:57Naibu Mkaguzi wa Kituo cha Kijeshi cha Khatam al-Anbiya amezungumzia makubaliano ya usitishaji vita kati ya HAMAS na utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa, makubaliano hayo yanatokana na Marekani na utawala wa Kizayuni kukata tamaa kwa sababu wamechoshwa mno na vita visivyo na mwisho licha ya jinai kubwa walizofanya Ukanda wa Ghaza.
-
Waziri: Mamilioni ya watalii wameitebelea Iran ndani ya miezi 6
Oct 16, 2025 02:08Zaidi ya watalii milioni 3.5 wa kigeni wameitembelea Iran katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu, Waziri wa Turathi za Utamaduni, Utalii na Sanaa, Reza Salehi Amiri alisema hayo jana Jumatano.