-
UN yaituhumu RSF kuwa imefanya "uhalifu wa kivita" huko El Fasher
Feb 14, 2026 02:50Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kwamba uhalifu unaofanywa na wapiganaji wa kundi la Rapid Support Forces (RSF) huko El Fasher nchini Sudan ni sawa na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.
-
Guardiola awatetea wahamiaji akijibu matamshi ya kibaguzi ya mmiliki wa Manchester United
Feb 14, 2026 02:27Meneja wa timu ya Manchester City, Pep Guardiola, amejibu maoni ya mmiliki wa Manchester United, Sir Jim Ratcliffe kuhusu uhamiaji, akisema kwamba kuna haja ya "kukumbatia tamaduni zingine ili kuifanya jamii iwe bora."
-
Palestine Action yapata ushindi muhimu wa kisheria dhidi ya ukandamizaji wa serikali ya Uingereza
Feb 14, 2026 01:01Mahakama Kuu ya Uingereza imetoa pigo kubwa la kisheria kwa jitihada za serikali ya nchi hiyo za kunyamazisha uungaji mkono wa wazi watu kwa Palestina, baada ya kutoa uamuzi kwamba hatua ya Wizara Mambo ya Ndani wa 2025 ya kupiga marufuku kundi la linalounga mkono Palestina la Palestine Action kwa madai kwamba ni shirika la kigaidi, ulikuwa kinyume cha sheria.
-
Al Houthi: Iran ni ngome imara inayokwamisha njama za Marekani na Israel
Feb 14, 2026 00:44Kiongozi wa harakati ya Kiislamu ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi.
-
Chama cha Jamaat-e-Islami nchini Bangladesh chatilia shaka matokeo ya uchaguzi
Feb 13, 2026 22:53Chama cha Jamaat-e-Islami, chama kikubwa zaidi cha Kiislamu nchini Bangladesh, kimehoji matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini humo majuzi, ambapo kimeshika nafasi ya pili kwa kupata viti 74 baada ya Chama cha Kizalendo cha Bangladesh, ambacho kumeshinda viti 212 kati ya 300 vya Bunge.
-
Iran yalaani juhudi za Israel za kunyakua Ukingo wa Magharibi, yasema ni 'maangamizi ya kizazi ya kikoloni'
Feb 13, 2026 22:53Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala ghasibu wa Israel wa kunyakua ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikisema hatua hiyo inalenga kupanua 'ujenzi wa vitongoji haramu' na kuimarish uvamizi na udhibiti wa masuala ya usalama katika eneo hilo, sambamba na kuendeleza 'mauaji ya kimbari' ya Gaza.
-
Rais wa mpito wa Venezuela: Maduro bado ndiye rais halali
Feb 13, 2026 22:52Rais wa mpito wa Venezuela, Delcy Rodríguez, amesema kwamba anaongoza nchi hiyo kwa kuzingatia vifungu vya Katiba, akikanusha madai kwamba Marekani inaendesha Venezuela, huku akisisitiza kwamba Nicolas Maduro anasalia kuwa rais halali wa jamhuri hiyo.
-
Machungu ya ukoloni; safari za kifo na jinai za kikatili za Ufaransa nchini Madagascar
Feb 13, 2026 22:48Madagascar, kisiwa kikubwa zaidi barani Afrika na makao ya jamii ya Malagasy, iliingia katika moja ya vipindi vya giza zaidi katika historia yake mwishoni mwa karne ya 19.
-
Kwa nini Grossi amekiri haki ya Iran ya kurutubisha urani?
Feb 13, 2026 07:51Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amekiri kwamba, Iran kama nchi iliyotia saini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ina haki ya kurutubisha urani.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Nchi tatu za Ulaya zilishiriki katika ghasia za Iran
Feb 13, 2026 07:19Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa nchi tatu za Ulaya, yaani Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani, zimehusika katika uchochezi na machafuko ya karibuni dhidi ya Iran. Amesema kwamba, kwa mtazamo wa wananchi wa Iran, nchi hizo zimeshirikiana na watenda jinai wakuu katika machafuko hayo.