Watu wasiopungua 31 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika miripuko ya mabomu iliyotokea usiku wa kuamkia leo kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwakomboa watu 148, wakiwemo wanawake 58 na watoto 75, ambao walikuwa wametekwa nyara na kundi la magaidi wakufurishaji la Boko Haram.
Mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika eneo la magharibi mwa Afrika ametangaza kuwa, licha ya kuweko mafanikio katika kupambana na kundi la kigaidi la Boko Haram, lakini itachukua miaka kadhaa ili kuliangamiza kikamilifu kundi hilo.
Jeshi la Nigeria limesema hivi karibuni lilifanikiwa kuwaokoa mateka wapatao elfu 1 kutoka kwa kundi lenye msimamo mkali la Boko Haram katika jimbo la Borno.
Magaidi wakufurishaji wa kundi la Boko Haram nchini Nigeria wamewateka watoto zaidi ya 1,000 tokea mwaka 2013.
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, limewakomboa mateka 149 kutoka mikononi mwa kundi la kigaidi la Boko Haram.
Duru za habari nchini Nigeria zimeripoti kwamba, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Boko Haram limefanya shambulizi katika mji wa Maiduguri, makao makuu ya jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Waziri wa Habari wa Nigeria amesema serikali inafanya mazungumzo na kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram kuhusu uwezekano wa kusitisha mapigano, lengo kuu likiwa ni kuhitimisha kikamilifu uadui na uhasama baina ya pande mbili.
Duru za kijeshi za Chad zimetangaza habari ya kutokea mapigano kati ya jeshi la nchi hiyo na magaidi wa Boko Haram katika eneo la Ziwa Chad.
Kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limewaachia huru mabinti 100 kati ya 110 iliowateka nyara mwezi uliopita wa Februari, kaskazini mashariki mwa nchi.