Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limewaua wanamgambo tisa wa kundi la kigaidi la Boko Haram katika mapigano yaliyotokea kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Wizara ya Ulinzi ya Niger imetangaza habari ya kuuawa makumi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram katika operesheni za jeshi la nchi hiyo huko kusini mashariki mwa nchi.
Jeshi la Nigeria limefanikiwa kuwakomboa raia 72 waliokuwa wakishikiliwa mateka na kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno.
Msemaji wa jeshi la Chad ametangaza kuwa jeshi hilo limewaangamiza magaidi elfu moja wa kundi la Boko Haram huko Magharibi mwa nchi hiyo.
Serikali ya Chad imetangaza kuwa magaidi wote wa kundi la Boko Haram wameshatokomezwa na kutimuliwa katika ardhi ya nchi hiyo.
Serikali ya Nigeria imetangaza kuwa kwa akali wanachama 100 wa kundi la kigaidi la Boko Haram wameangamizwa katika operesheni dhidi ya ugaidi iliyotekelezwa na jeshi la nchi hiyo.
Wizara ya Ulinzi ya Nigeria imethibitisha habari za kuangamizwa makamanda wa ngazi za juu na wanachama kadhaa wa kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi.
Magaidi wakufurishaji wa kundi la Boko Haram wameshambulia kijiji magharibi mwa Chad na kuwaua wanakijiji kadhaa na kuwateka nyara wanawake.
Kwa akali watu 30 wameuawa huku makumi ya wengine wakijeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea karibu na daraja lenye shughuli nyingi katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Maafisa usalama wa Cameroon wametangaza kuwa raia wawili wameuawa katika shambulio la kigaidi la kundi la Boko Haram katika eneo la kaskazini ya mbali nchini humo.