-
Khartoum yatoa ushahidi dhidi ya UAE na kuikosoa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
Jul 18, 2026 09:07Waziri wa Sheria wa Sudan, Abdullah Darf, amewasilisha kifurushi cha njia za kisheria "zisizo za kawaida" ambazo serikali ya Khartoum inakusudia kuchukua ili kufungua mashtaka dhidi ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF), akisisitiza kwamba Khartoum ina "ushahidi wa kutosha na data kamili" kuhusu "ushiriki wa Abu Dhabi katika vita na uhalifu uliofanywa na pande hizo mbili dhidi ya watu wa Sudan."
-
Gavana wa Darfur: Katika kipindi cha siku tatu tu, RSF iliua Wasudan 27,000 El-Fasher
Nov 26, 2025 07:21Gavana wa Jimbo la Darfur nchini Sudan, Minni Arko Minnawi, ameviambia vyombo vya habari kuwa, katika kipindi cha siku tatu tu Wasudan 27,000 waliuliwa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) wakati wanamgambo wa vikosi hivyo walipoendeleza wimbi la mauaji baada ya kuuteka mji wa el-Fasher mwishoni mwa mwezi uliopita.
-
RSF imezika kwa halaiki na kuchoma moto maiti za mamia ya raia El-Fasher kuficha jinai za mauaji ya kimbari
Nov 10, 2025 02:48Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa, maiti za mamia ya raia zimezikwa katika makaburi ya pamoja na nyingine zimechomwa moto na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) mjini El-Fasher magharibi mwa nchi hiyo.
-
Mtandao wa Madaktari Sudan: RSF imeteketeza mamia ya miili ya watu huko El Fasher
Nov 09, 2025 06:34Mtandao wa Madaktari wa Sudan umesema kwamba Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilikusanya mamia ya miili kutoka mitaani na vitongoji vya makazi ya raia vya El Fasher (mji mkuu wa Darfur Kaskazini) na kuzika baadhi ya miili hiyo katika makaburi ya umati, huku mingine ikichomwa moto kabisa.
-
Balozi wa Russia nchini Sudan: Mamluki wa Ukraine wanaendeshaji droni huko Darfur
Nov 08, 2025 03:45Balozi wa Russia nchini Sudan, Andrey Chernovol, ameripoti kwamba kuna uvumi unaosambaa nchini Sudan kuhusu uwepo wa Waukreini wanasimamia operesheni za ndege zisizo na rubani katika safu ya waasi wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF).
-
El Fasher, Hadithi ya Kuanguka Mji
Nov 07, 2025 13:02El Fasher sio jina la mji tu; bali ni jeraha lililowazi la dhamiri ya dunia. Katika kipindi chetu leo, tunasimulia mzingiro uliozuia mkate wa watu, na hujuma iliokata pumzi za watoto. Ni simulizi fupi lakini sahihi, inayotuhimiza sisi sote kuelekeza mazingatio yetu kwa maafa ya binadamu yanayotokea huko Sudan....
-
Watoto wanakufa kwa njaa katika jimbo la Darfur, Sudan huku ugonjwa wa Kipindupindu ukienea
Jul 30, 2025 09:14Watoto 13 wameaga dunia kutokana na njaa katika kambi ya raia waliokimbia makazi yao katika jimbo la Darfur Mashariki nchini Sudan.
-
Mashambulio ya siku tatu mtawalia ya RSF yaua watu 450 Darfur, magharibi mwa Sudan
Apr 14, 2025 02:41Harakati ya Jeshi la Ukombozi wa Sudan, inayoongozwa na Minni Arko Minnawi (SLA-Minnawi), gavana wa jimbo la Darfur magharibi mwa nchi hiyo, imetangaza kuwa watu 450 wameuawa kutokana na mashambulizi ya siku ya tatu mtawalia yaliyofanywa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) katika mji wa El Fasher, makao makuu ya eneo hilo, na kwenye kambi za wakimbizi.
-
UNICEF: Machafuko na njaa vinatishia maisha ya maelfu ya watoto wa Sudan
Mar 28, 2025 23:41Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetangaza kuwa, ghasia na njaa vinatishia maisha ya watoto wa Sudan hususan katika mzozo wa jimbo la Darfur Kaskazini.
-
Ripoti ya UN: RSF inashambulia na kuua raia Darfur, Sudan kwa msingi wa ukabila
Mar 01, 2024 23:38Ripoti mpya ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa imesema, Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF pamoja na wanamgambo vinaoshirikiana nao wanaopigania kutwaa madaraka nchini Sudan wamefanya mauaji ya kikabila na ubakaji wakati wa udhibiti wa eneo kubwa la Darfur magharibi mwa nchi hiyo, na kwamba vitendo hivyo vinaweza kuwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.