-
Ethiopia yatetea oparesheni za kijeshi Tigray, yasema lengo ni kuokoa taifa
Nov 11, 2020 04:36Ethiopia imetetea operesheni ya kijeshi inayoendelea katika sehemu ya kaskazini mwa nchi hiyo na kusema oparesheni hiyo inalenga kuokoa taifa.
-
Waethiopia waanza kumiminika Sudan wakikimbia vita, wamo wanajeshi wa serikali
Nov 10, 2020 06:49Serikali ya Sudan imetangaza kuwa makumi ya wakimbizi kutoka Ethiopia wamevuka mpaka na kuingia kusini mashariki mwa nchi hiyo. Taarifa ya serikali ya Sudan imesema kuwa wakimbizi hao ambao wanajumuisha wanajeshi 30 wa serikali ya Ethiopia, wameingia katika eneo la Al-Luqdi mashariki mwa jimbo la al-Qadarif.
-
Wakazi wa Amhara nchini Ethiopia waunga mkono oparesheni ya jeshi huko Tigray
Nov 09, 2020 08:57Wakazi wa jimbo la Amhara kaskazini mwa Ethiopia linalopakana na eneo la Tigray wamesema kuwa wapo tayari kuliunga mkono jeshi la ulinzi ya nchi hiyo katika mzozo na harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF).
-
Waziri wa Mambo ya Nje, Mkuu wa Ujasusi, kamanda wa jeshi, watimuliwa Ethiopia
Nov 09, 2020 01:13Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed jana Jumapili aliwafuta kazi Waziri wa Mambo ya Nje, mkuu wa shirika la kijasusi la nchi hiyo na kamanda wa jeshi la nchi hiyo.
-
Bunge la Ethiopia laafiki kuundwa serikali katika eneo la Tigray
Nov 07, 2020 07:24Baada ya mapigano makali ya hivi karibuni baina ya vikosi vya serikali ya Ethiopia na vile vya Harakati ya Wananchi ya Ukombozi wa Tigray (The Tigray People's Liberation Front (TPLF), hatimaye Bunge la nchi hiyo limeafiki kuundwa serikali ya muda katika eneo hilo.
-
Ethiopia yasema uasi Tigray unachochewa na madola ya kigeni
Nov 06, 2020 07:55Serikali ya Ethiopia imesema imeamua kutumia nguvu za kijeshi katika eneo la Tigray baada ya kupokea taarifa za kijasusi kuwa serikali yenye mamlaka ya ndani ya eneo hilo inapokea misaada ya kigeni kuchukua hatua dhidi ya serikali kuu iliyoko Addis Ababa.
-
Sudan yafunga mpaka wake baada ya Ethiopia kutangaza vita na waasi
Nov 06, 2020 03:06Viongozi wa serikali ya Sudan katika jimbo la Kassala wamefunga mpaka wao na Ethiopia baada ya Addis Ababa kutangaza vita na waasi wanaopigania kujitenga eneo la Tigray.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia: Jeshi limefanikiwa dhidi ya harakati ya TPLF
Nov 05, 2020 04:31Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia amesema kuwa mashambulizi ya Harakati ya Wananchi ya Ukombozi wa Tigray (The Tigray People's Liberation Front (TPLF)) yamedhibitiwa. Amesema jeshi la Ethiopia litatekeleza oparesheni nyingine siku chache zijazo.
-
Kwa amri ya Abiy Ahmed: Jeshi la Ethiopia laanza mashambulizi dhidi ya harakati ya TPLF
Nov 04, 2020 05:24Jeshi la Ethiopia mapema leo limeanza mashambulizi dhidi ya Harakati ya Wananchi ya Ukombozi wa Tigray (The Tigray People's Liberation Front (TPLF)).
-
Makumi wauawa katika shambulio la wabeba silaha Ethiopia
Nov 03, 2020 03:39Makumi ya watu wameuawa katika shambulizi la wanamgambo waliobeba silaha magharibi mwa Ethiopia.