Marekani inatazamiwa kutoa ishara leo Jumanne juu ya uwezekano wa kujiondoa kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuukingia kifua utawala haramu wa Israel.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limekosoa vikali jinai, ukandamizaji, ubaguzi na ukaliwaji wa mabavu wa ardhi za Palestina na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa zaidi ya miongo mitano sasa.
Mkuu wa Kamisheni ya Haki za Binaadamu barani Ulaya amesema kuwa, haki za binaadamu zilianzia nchini Iran hususan mji wa Shiraz (kusini wa nchi) uliokuwa mji mkuu wa utamaduni wa dunia.
Rais Mahamadou Issoufou wa Niger ametoa wito wa kuchukuliwa hatua madhubuti kwa ajili ya kukabiliana na ukosefu wa usalama na wakati huo huo kuungwa mkono suala la haki za binadamu barani Afrika.
Kikao cha sitini cha Kamisheni ya Haki za Binadamu na Watu ya Umoja wa Afrika (ACHPR) kimeanza katika mji mkuu wa Niger, Niamey kwa kuhudhuriwa na wawakilishi zaidi ya 600 kutoka nchi mbalimbali za Afrika na za mabara mengine duniani. Kikao hicho kilianza siku ya Jumatatu ya tarehe 8 Mei na kitaendelea kwa muda wa wiki mbili hadi tarehe 22 mwezi huu.
Makundi ya haki za binadamu katika kona mbalimbali za dunia yamelaani jinai za ukoo wa Aal Khalifa dhidi ya wafungwa nchini Bahrain na kuutaka utawala huo kandamizi kuacha kuwanyanyasa wafungwa.
Waziri Mkuu wa Ubelgiji amesema nchi hiyo ya Ulaya inajuta kwa kuiunga mkono Saudi Arabia kupewa uanachama wa Kamati ya Haki za Wanawake ya Umoja wa Mataifa.
Kongamano la Kimataifa la Kiislamu kuhusu Haki za Binadamu linafanyika hapa nchini Iran katika Chuo Kikuu cha Tehran.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limelaani vikali hatua ya Marekani ya kukishambulia kituo cha kijeshi cha Syria kwa makombora na kusisitiza kuwa 'mashambulizi hayo ya jazba' sio njia mbadala ya kufanyika uchunguzi wa kina juu ya mashambulizi ya silaha za kemikali katika eneo la Khan Sheikhoun.
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kusikitishwa kwake na wito wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kutaka kurejeshwa sheria ya kuwatesa watuhumiwa wa jinai mbalimbali.