-
Haki za binadamu; chombo cha kisiasa cha Magharibi kwa ajili ya kuishinikiza Iran
Dec 19, 2020 07:17Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kupitishwa azimio lililo dhidi ya Iran katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hakuna itibari yoyote ya kisheria na kwamba waliobuni azimio hilo wanazitumia vibaya taasisi za kimataifa.
-
Kupaswisha azimio dhidi ya Iran katika Bunge la Ulaya
Dec 18, 2020 03:11Wabunge wa Umoja wa Ulaya jana Alkhamisi walipasisha azimio linaloituhumu Iran kuwa inakiuka haki za binadamu
-
Mkuu wa IAEA: Iran inataka kuona dunia yenye usalama na uthabiti
Dec 17, 2020 04:08Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema hamu kubwa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kuona usalama na uthabiti vinatawala duniani kote, na kwamba Tehran iko tayari kufanya mazungumzo amilifu na mataifa ambayo yapo tayari kufuata njia ya mazungumzo.
-
Iran yaitaka Marekani iondoe askari wake vamizi nchini Syria
Dec 17, 2020 04:01Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema vikosi vamizi vya nchi ajinabi vikiweko vya Marekani vinapaswa kuondoka nchini Syria mara moja.
-
Viongozi wa Marekani waendeleza misimamo yao ya kiuadui dhidi ya Iran
Dec 15, 2020 04:38Ikiwa ni katika kudumisha misimamo ya uhasama ya viongozi wa White House dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, mjumbe maalumu wa serikali ya Marekani anayeshughulikia masuala ya Iran ameunga mkono vikwazo vya Washington dhidi ya Tehran.
-
Zanganeh: Iran haihitaji idhini ya kurejea katika soko la mafuta
Dec 14, 2020 08:57Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Bijan Namdar Zangeneh amesema taifa hili halihitaji idhini yoyote kurejea katika soko la mafuta na kwamba lina uwezo wa kuuza mapipa milioni 2.3 ya mafuta kila siku.
-
Iran yalalamikia taarifa ya Ufaransa ya kumuunga mkono mhalifu aliyenyongwa
Dec 14, 2020 01:20Iran imemuita balozi wa Ufaransa mjini Tehran Philippe Thiebaud kulalamikia taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo ya Ulaya ambayo imelaani kutekelezwa hukumu ya kunyongwa Ruhullah Zam, aliyepatikana na hatia ya kusimamia mtandao uliokuwa ukiendesha propaganda chafu dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Iran: Marekani inawashawishi wengine watoe muhanga kadhia ya Palestina
Dec 12, 2020 03:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema Marekani inazishawishi nchi zingine kutoa muhanga kadhia ya Palestina na kuwapa mkono wezi kwa njia mbali mbali.
-
Kinara wa propaganda za ghasia anyongwa Iran
Dec 12, 2020 03:37Ruhullah Zam, kinara wa mtandao wa habari wa Amad News ambao ulikuwa unaeneza propagadna dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu amenyongwa kufuatia hukumu iliyotoelwa na mahakama.
-
Watu 232 wengine wafariki dunia kwa corona nchini Iran
Dec 11, 2020 09:54Msemaji wa Wizara ya Afya, Tiba na Mafunzo ya Utabibu ya Iran amesema kuwa, watu wengine zaidi ya elfu 9 wameambukizwa kirusi cha corona na wengine 232 wamefariki dunia katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.