-
Iran: Uropokaji mpya wa Marekani unakusudia kuipotosha dunia
Apr 19, 2020 03:22Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Marekani imeazimia kuupotosha ulimwengu, ili usishughulishwe tena na ugaidi wa kiuchumi wa taifa hilo la kibeberu dhidi ya Iran.
-
"Gwaride la Huduma": Jeshi la Iran liko pamoja na wananchi katika vita dhidi ya corona
Apr 17, 2020 05:05Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran daima hulinda kiwango cha uwezo wake wa kiulinzi na kumzuia adui kuanzisha mashambulizi na wakati huo huo huwa pamoja na wananchi wakati wa maafa au majanga na kuwasaidia kutatua matatizo yao.
-
Madai ya kushangaza ya Saudia; serikali ya Mansur Hadi inaihudumia Iran
Apr 17, 2020 02:34Siku ya Jumatano Muhammad Aal Jabir, balozi wa Saudi Arabia nchini Yemen alimtuhumu Ahmed Saleh Al-Issa, naibu mkuu wa masuala ya kiuchumi wa ofisi ya Abdurabbuh Mansur Hadi, rais aliyestaafu na kukimbia nchi wa Yemen kuwa anaiuzia mafuta Iran.
-
Jeshi la Majini la Iran kuunda nyambizi za nyuklia
Apr 17, 2020 00:00Kamanda wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kikosi hicho kinajiandaa kuunda nyambizi zitakazotumia nishati ya nyuklia zenye uwezo wa kutekeleza operesheni za baharini kwa muda mrefu zaidi katika maji ya kimataifa.
-
Tahadhari ya Russia kuhusiana na kuutumia kisiasa mgogoro wa corona
Apr 16, 2020 23:53Katika kipindi hiki cha mgogoro wa mlipuko wa virusi vya corona, Marekani ambayo ni kinara wa nchi za Magharibi imeendeleza siasa zake zisizo za kibinadamu dhidi ya nchi hasimu na wapinzani wake, hususn katika kuzidisha vikwazo vya kiuchumi na kuzizuia kupata misaada ya kimataifa. Suala hili limekosolewa sana na madola mengine makubwa duniani.
-
Tuhuma za ajabu, Saudia yamtuhumu kibaraka wake kuwa anaisaidia Iran kuuza mafuta yake
Apr 16, 2020 03:16Mohammed bin Saeed Aal Jabir, balozi wa Saudi Arabia nchini Yemen, jana alimtuhumu afisa mmoja wa ngazi za juu wa serikali ya Abdu Rabbuh Mansour Hadi, rais wa zamani wa Yemen aliyejiuzulu na kukimbilia Saudia kwamba anashiriki katika kuiuzia Iran mafuta yake.
-
Kwa mara nyingine UN yaitaka Marekani iondoe vikwazo vyake duniani wakati huu wa corona
Apr 16, 2020 03:12Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine ametilia mkazo mwito wa umoja huo wa kuitaka Marekani ifute vikwazo vyake kwa mataifa ya dunia wakati huu wa vita dhidi ya COVID-19.
-
Bunge la Juu ya Uingereza lataka kuondolewa vikwazo Iran
Apr 15, 2020 03:39Mwenyekiti wa Kamati ya Uhusiano wa Kimataifa na Ulinzi ya Bunge la Juu la Uingereza (House of Lords) amesema anaunga mkono miito inayotolewa na maafisa wa nchi za Ulaya na Marekani za kutaka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iondolewa vikwazo, katika kipindi hiki ambapo Iran inaendelea kukabiliana na maambukizi makubwa ya virusi vya Corona.
-
Kukabiliana na Corona; Changamoto za kimataifa za kuokoa maisha ya wanadamu
Apr 15, 2020 03:13Kuhatarisha afya ya watu kwa malengo ya kisiaisa si tu kuwa ni kinyume cha sheria bali ni ukatili. Hiyo ni kauli ya madakatari na wataalamu 550 wanachama wa Baraza la Kitiba la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambao wamemuandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kubainisha nukta hiyo huku wakilalamikia kuendelea sera za vikwazo vya Marekani dhidi ya taifa la Iran.
-
Baraza la Makanisa Duniani laitaka Marekani iiondolee Iran vikwazo
Apr 12, 2020 23:06Baraza la Makanisa Duniani na Jumuiya ya Kitaifa ya Makanisa ya Kristo zimeeleza wasiwasi wao juu ya athari mbaya za vikwazo vya Marekani dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.