-
Vipaumbele muhimu zaidi vya sera za kigeni za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
May 11, 2025 04:29Seyyed Abbas Araghchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefafanua vipaumbele na masuala muhimu zaidi katika siasa za nje za Iran katika kikao cha Doha na pia katika vikao vingine na viongozi mbalimbali wa nchi za eneo.
-
Ni vipi vipaumbele vya Iran katika Duru ya 4 ya Mkutano wa Mazungumzo kati ya Iran na Nchi za Kiarabu
May 10, 2025 08:02Duru ya 4 ya Mkutano wa Mazungumzo kati ya Iran na Nchi za Kiarabu chini ya anwani "Uhusiano Imara na Maslahi ya Pande Mbili" inafanyika Doha mji mkuu wa Qatar kwa ushirikiano wa pamoja wa Baraza la Kiistratejia la Uhusiano wa Nje la Iran na Kituo cha Utafiti cha al Jazira.
-
Makamu wa Rais wa Marekani: Vita vya India na Pakistan 'havituhusu'
May 09, 2025 04:17Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amesema, nchi hiyo haitaingilia mzozo kati ya India na Pakistan.
-
Je, Dan Jarvis anasema nini? Ni nani na amefanya nini?
May 08, 2025 22:50Madai yaliyotolewa katika bunge la Uingereza siku ya Jumanne, Mei 6 na Dan Jarvis, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo, kwa mara nyingine tena yameibua kile kinachodaiwa kuwa tishio la usalama kutoka Iran.
-
Iran yakaribisha upatanishi wa Oman uliopelekea US kusitisha mashambulizi dhidi ya Yemen
May 08, 2025 03:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amekaribisha taarifa ya Oman kuhusu kusitishwa kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya Yemen, akisema kuwa nchi za eneo hili hazitasahau Muqawama wa watu wa Yemen dhidi ya uvamizi wa kigeni.
-
Araqchi atahadharisha kuhusu ghadhabu ya Wairani ikiwa Trump atabadlisha jina la Ghuba ya Uajemi
May 07, 2025 23:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametahadharisha kuhusu ghadhabu ya Wairani wote baada ya tetesi kwamba Rais Donald Trump wa Marekani ana mpango wa kubadili jina la Ghuba ya Uajemi katika ziara yake nchini Saudi Arabia, wiki ijayo.
-
Jibu la mkato la Iran kwa porojo la Netanyahu
May 07, 2025 05:28Amir-Saeid Iravani, Balozi na Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameliandikia barua Baraza la Usalama la umoja huo kujibu porojo na upayukaji wa waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni Benjamin Netanyahu dhidi ya Iran.
-
Msemaji wa serikali ya Iran: Vikwazo vya Marekani vinalenga maisha ya raia
May 07, 2025 03:04Msemaji wa Serikali ya Iran amesema kuwa vikwazo vilivyowekwa na serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vinaathiri maisha ya watu wa kawaida.
-
Iran yalaani shambulio dhidi ya Port Sudan lililoua mamia ya watu
May 04, 2025 22:54Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani shambulizi la ndege isiyo na rubani ambalo lililenga uwanja wa ndege pamoja na maeneo na vituo vya kiraia mashariki mwa Sudan.
-
Makosa 6 makubwa ya kimkakati ya Marekani kuhusu Iran
May 04, 2025 22:52Baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kuasisiwa Jamhuri ya Kiislamu nchini Iran, Marekani ikiwa kiongozi wa nchi za Magharibi, muda wote imekuwa ikilifanyia uadui taifa la Iran katika kipindi cha miaka 46 sasa ikiwa ni pamoja na kuliwekea vikwazo vikubwa kupindukia. Hata hivyo Washington imeshindwa kufikia malengo yake dhidi ya Iran.