-
Iran na nchi tatu za Ulaya zaafikiana kuendeleza mazungumzo ya kidiplomasia
Nov 30, 2024 03:58Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran wa masuala ya Sheria na Kimataifa amesema Jamhuri ya Kiislamu na nchi tatu za Ulaya zimeafikiana kuendeleza mazungumzo ya kidiplomasia.
-
Iran yawataka wasomi wa Kiislamu kuzuia dhulma dhidi ya Waislamu huko Palestina na Lebanon
Nov 28, 2024 07:57Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amewataka wanazuoni wa Ulimwengu wa Kiislamu kuwatetea watu wanaodhulumiwa na Waislamu kote duniani, na pia kuchukua maamuzi ya kijasiri ya kusitisha ukatili na jinai zinazofanyika katika Ukanda wa Gaza na Lebanon.
-
Hizbullah yaishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa himaya yake ya pande zote
Nov 28, 2024 07:56Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imemshukuru Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kutokana na himaya yake na hatua za kidiplomasia za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran za kusimamisha vita nchini Lebanon.
-
Iran na Algeria zatilia mkazo udharura wa kushirikiana kupambana na Israel
Nov 25, 2024 22:57Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Algeria na pande mbili zimetilia mkazo udharura wa kushirikiana mabunge ya nchi zao kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza na Lebanon.
-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran aahidi uungaji mkono endelevu kwa Muqawama
Nov 25, 2024 07:48Israel imefikia katika hali ya mkwamo, na Jamhuri ya Kiislamu itaendelea daima kuunga mkono mapambano halali na ya haki dhidi ya utawala wa kibaguzi wa Israel.
-
Araghchi kushiriki mkutano wa UNAOC nchini Ureno
Nov 25, 2024 00:21Abbas Araghchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anatazamia kuelekea nchini Ureno kushiriki katika mkutano wa 10 wa kimataifa wa Kongamano la Muungano wa Umoja wa Mataifa wa Ustaarabu (UNAOC).
-
SEPAH: Magaidi 88 wameangamizwa na kutiwa mbaroni kusini mashariki mwa Iran + Video
Nov 24, 2024 03:58Msemaji wa luteka ya kijeshi ya kambi ya Quds ya Jeshi la Nchi Kavu la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ametangaza habari ya kuangamizwa na kutiwa mbaroni magaidi 88 katika mazoezi ya kijeshi ya mashahidi wa usalama kwenye mkoa wa Sistan na Baluchistan wa kusini mashariki mwa Iran.
-
Iran na Qatar zasisitiza ulazima wa kuhitimishwa mauaji ya kimbari Ukanda wa Gaza
Nov 21, 2024 04:27Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar katika mazungumzo yao mjini Tehran wamesisitiza juu ya ulazima wa kukomeshwa mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.
-
Kikao cha pili cha kamati ya pande tatu za Iran, Saudi Arabia na China chafanyika Riyadh
Nov 20, 2024 08:26Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Saudi Arabia na China zimefanya kikao cha pili cha pande tatu huko Riyadh, Saudi Arabia kwa shabaha ya kufuatilia makubaliano yaliyofikiwa huko Beijing na kuimarisha kiwango cha ushirikiano.
-
Iran: Ni muhimu kuwepo mshikamano wa kimataifa kwa ajili ya kuwahami wanawake na watoto wa Gaza na Lebanon
Nov 20, 2024 08:13Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayehusika na masuala ya wanawake na familia amesisitiza umuhimu wa mshikamano wa kimataifa kwa ajili ya kuwahami na kuwasaidia wanawake na watoto wa Gaza na Lebanon.