-
UN: Kombora la balestiki la Korea Kaskazini limetumika kushambulia mji wa Kharkiv, Ukraine
Apr 30, 2024 07:21Wachunguzi wa vikwazo wa Umoja wa Mataifa wameiambia kamati ya vikwazo ya Baraza la Usalama la umoja huo kuwa, mabaki ya kombora yaliyopatikana katika mji wa Kharkiv nchini Ukraine mnamo Januari 2 yanatokana na kombora la balestiki la Korea Kaskazini aina ya Hwasong-11.
-
Kim atabiri: Mashambulio ya Israel yanaandaa mazingira ya kuzuka Vita vya Tatu vya Dunia
Oct 29, 2023 03:01Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema, mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina yanaandaa mazingira ya kuzuka Vita vya Tatu vya Dunia.
-
Pyongyang: Israel imefanya jinai ya kivita kwa kushambulia hospitali Gaza
Oct 27, 2023 02:30Korea Kaskazini imelaani vikali shambulio la anga lililofanywa na jeshi la utawala haramu wa Israel dhidi ya Hospitali ya Al Ahli Arab katika Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 17 na kuua mamia ya wananchi wa Paalestina.
-
Balozi wa Korea Kaskazini nchini Russia: Marekani itashindwa huko Ukraine kama ilivyofeli Afghanistan
Oct 22, 2023 03:20Balozi wa Korea Kaskazini nchini Russia amelaani uungaji mkono na misaada ya kijeshi ya Marekani kwa Ukraine na kusema, mara hii pia Marekani itashindwa na kufeli kama ilivyokuwa huko Afghanistan.
-
Ushirikiano wa Korea Kaskazini na Russia dhidi ya Marekani
Oct 21, 2023 11:28Katika mazungumzo yake na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, Sergei Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, wamejadiliana kuhusu uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wao wa hivi sasa na kusisitiza juu ya makubaliano yao ya kutatua kidiplomasia masuala yenye utata katika Peninsula ya Korea.
-
Korea Kaskazini yatishia kuishambulia manowari ya kubebea ndege za kivita ya Marekani
Oct 15, 2023 02:32Korea Kaskazini imeitishia Marekani kwamba itaanzisha "shambulio kali zaidi na la haraka zaidi la kujikinga" dhidi ya zana za kijeshi za nchi hiyo, ikiwa ni pamoja na meli yake ya kivita ya nyuklia iliyoko kwenye maji ya Peninsula ya Korea.
-
Pyongyang: Askari wa US alitorokea Korea Kaskazini kutokana na ubaguzi
Aug 17, 2023 03:13Serikali ya Pyongyang imesema askari Mmarekani mwenye asili ya Afrika alitorokea Korea Kaskazini kutokana na vitendo vya ubaguzi wa rangi na dhulma alizokuwa akishuhudia ndani ya jeshi la Marekani.
-
Putin na Kim watilia mkazo kuwepo uhusiano wa karibu zaidi kati ya Russia na Korea Kaskazini
Aug 16, 2023 02:48Rais Vladimir Putin wa Russia na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wameahidi kujenga ushirikiano wa karibu zaidi kati ya nchi zao mbili katika mawasiliano waliyofanya kwa barua kwa manasaba wa maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Ukombozi wa Korea Kaskazini.
-
Korea Kaskazini yakosoa msaada wa silaha za Marekani kwa Taiwan
Aug 04, 2023 07:51Korea Kaskazini imekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuipa Taiwan msaada wa silaha wa mamilioni ya dola ikisisitiza kuwa, Washington inakitumia kisiwa hicho kinachojitawala kushadidisha taharuki na kuchochea moto wa vita katika eneo.
-
Korea Kaskazini yavurumisha makombora kujibu uchokozi wa Marekani
Jul 19, 2023 10:09Korea Kaskazini imevurumisha makombora mawili ya balestiki kuelekea Bahari ya Mashariki kujibu chokochoko za Marekani.