-
Mazungumzo ya Doha yamalizika, pande husika zaahidi kudumisha mawasiliano
Jun 30, 2022 03:45Mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana kati ya Iran na Marekani kuhusu uondoaji vikwazo yaliyoanza juzi Jumanne katika mji mkuu wa Qatar, Doha yamemalizika; huku pande mbili zikisema kuwa zitaendelea kuwasiliana juu ya marhala zijazo za mazungumzo hayo.
-
Raisi: Vikwazo vipya vinaonesha Iran ina haki ya kutoiamini Marekani
Jun 17, 2022 07:25Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya Marekani kwa upande mmoja kudai kuwa ina nia ya kweli ya kufanya mazungumzo na Iran na wakati huohuo inatangaza vikwazo vipya dhidi ya taifa hili kwa upande mwingine, inaonesha wazi kuwa Tehran ina haki kutoiamini Washington.
-
IMF: Vikwazo dhidi ya Russia yumkini vitadhoofisha dola ya US
Mar 31, 2022 22:55Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeonya kuwa, vikwazo dhidi ya Russia huenda vikadhoofisha na kuipotezea umashuhuri sarafu ya dola ya Kimarekani.
-
Ershadi: Vikwazo vinatishia haki ya tiba ya wananchi wa Iran
Mar 30, 2022 02:16Balozi na Naibu Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema vikwazo vya upande mmoja vya Marekani ni tishio kubwa kwa haki ya kupata huduma za afya, matibabu na dawa wananchi wa Iran.
-
Shamkhani: Mashinikizo ya juu yamefelishwa na sera ya muqawama
Mar 03, 2022 22:59Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema stratejia ya muqawama amilifu ndiyo iliyoishinda na kusambaratisha sera ya mashinikizo ya kiwango cha juu zaidi ya aliyekuwa rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya Iran.
-
Raisi: Makubaliano yoyote ya Vienna sharti yajumuishe kuondolewa vikwazo Iran
Feb 20, 2022 00:18Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mapatano yoyote yatakayofikiwa kwenye mazungumzo ya Vienna yenye lengo la kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA lazima yajumuishe suala la kuondolewa vikwazo taifa la Iran, sanjari na kupasishwa kwa kipengee kuhusu dhamana yenye itibari, na vile vile kujizuia na masuala ya kisiasa na kuibua tuhuma zisizo na msingi.
-
Shamkhani: Mienendo hasi ya US ndilo tishio kuu kwa mapatano yoyote yale
Feb 15, 2022 23:17Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema siri ya kufikiwa mapatano mazuri kwenye mazungumzo ya kuiondolea vikwazo haramu Jamhuri ya Kiislamu ni Tehran kupewa dhamana ya kisheria ambayo itaifanya Marekani isiweze kujitoa kwa mara nyingine tena ndani ya mapatano ya JCPOA.
-
Iran: Kumalizika mazungumzo ya Vienna kunategemea kuondolewa vikwazo Tehran
Feb 10, 2022 23:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema muda wa kumalizika mazungumzo ya Vienna ya kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA unategemea irada ya Wamagharibi ambao ni upande wa pili wa mazungumzo hayo, kuiondolewa vikwazo haramu Tehran.
-
Marais wa Iran na Ufaransa wajadili suala la kuondolewa vikwazo Tehran
Jan 29, 2022 23:56Rais wa Iran amesisitiza juu ya udharura wa kuondolewa vikwazo wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu, katika mazungumzo yake ya simu na mwenzake wa Ufaransa.
-
Amir Abdollahian: Maslahi kamili ya Iran yanapasa kupatikana katika suala la kuondoa vikwazo
Jan 27, 2022 22:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa maslahi kamili ya Iran yanapasa kupatikana katika suala la kundolea vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.