-
Juhudi za Uturuki za kuweko kijeshi katika nchi ya Libya
Jun 14, 2020 08:08Baada ya Uturuki kuwa na uingiliaji wa kijeshi katika masuala ya ndani ya Libya na kushiriki pakubwa katika vita vya niaba, sasa viongozi wa Ankara wanazungumzi suala la kuanzisha vituo viwili vya kijeshi katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Umoja wa Mataifa wataka uchunguzi ufanyike kuhusu makaburi ya umati Libya
Jun 14, 2020 02:59Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameeleza kushtushwa kwake kutokana na kugundulika kwa makaburi ya umati nchini Libya katika siku za hivi karibuni, katika eneo ambalo hivi karibuni lilikuwa chini ya udhibiti wa wanamgambo wanaojiita Libyan National Army (LNA) ambao wanaoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Mufti wa Libya atoa fatwa ya kuharamisha bidhaa za Misri, UAE na Jordan
Jun 13, 2020 02:53Mufti wa Libya ametoa fatwa ya kuharamisha ununuzi wa bidhaa kutoka Misri, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Jordan.
-
Independent: Wafanyabiashara wa Kimagharibi wamemtapeli Haftar mamilioni ya dola
Jun 11, 2020 22:07Gazeti la Independent linalochapishwa nchini Uingereza limefuchua kwamba mamluki wa nchi za kigeni na wafanyabiashara wa nchi za Magharibi wakiwemo Waingereza, wamemtapeli jenerali muasi Khalifa Haftar mamilioni ya dola za Kimarekani.
-
17 wauawa na kujeruhiwa katika mlipuko wa bomu Tripoli, Libya
Jun 11, 2020 03:27Kwa akali watu saba wameuawa na wengine zaidi ya kumi wamejeruhiwa katika mlipuko wa bomu uliotokea karibu na mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
Gazeti la Qatar: Kumefikiwa makubaliano ya kimataifa ya kummaliza Khalifa Haftar wa Libya
Jun 10, 2020 21:55Gazeti la al Arabi al Jadid limeripoti habari ya kufikiwa makubliano ya kimataifa ya kummaliza kabisa kisiasa jenerali muasi Khalifa Haftar wa Libya.
-
Umoja wa Afrika wazitaka pande hasimu Libya kuzingatia sheria za kimataifa
Jun 10, 2020 07:39Mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat amezitaka pande zinazopigana nchini Libya zifuate sheria ya kibinadamu ya kimataifa, hasa kuhakikisha usalama wa hospitali na shule, na kuwezesha utoaji wa misaada.
-
UN yasisitiza ulazima wa kutatuliwa mgogoro wa Libya kwa njia za amani
Jun 09, 2020 03:04Uingiliaji kati wa nchi za kigeni katika mgogoro wa Libya umezidisha wasiwasi wa kimataifa kuhusu mgogoro huo. Katika mkondo huo Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake kuhusiana na hali ya Libya na umezitaka pande zote zinazohusika kuheshimu njia za kisiasa za kutatua mgogoro huo.
-
Morocco yapinga pendekezo la Misri kuhusu Libya
Jun 08, 2020 07:34Serikali ya Morocco imepinga mpango wa Misri kuhusu Libya na kusisitiza kuwa muafaka wa kisiasa wa al Sakhirat ni marejeo asili ya ufumbuzi wa mgogoro wa Libya.
-
Wapiganaji wa Haftar warejea nyuma kutoka mji wa Sirte nchini Libya
Jun 06, 2020 23:47Askari wa serikali ya mwafaka wa kitaifa yenye makao yake magharibi mwa Libya wameelezea habari ya kukimbia wanamgambo wanaoongozwa na Jenerali Khalifa Haftar kutoka katika mji wa Sirte hadi umbali wa kati ya Tripoli na Bengazi.