-
Wasudan waendeleza maandamano ya kushinikiza utawala wa kiraia
Apr 26, 2019 14:22Maelfu ya wananchi wa Sudan wamesali Sala ya Ijumaa nje ya makao makuu ya jeshi la nchi hiyo mjini Khartoum, siku moja baada ya maandamano makubwa kushuhudiwa katika kona mbalimbali za mji mkuu huo, kulishinikiza jeshi likabidhi madaraka kwa raia.
-
Raia wa Italia waandamana kuupinga utawala wa Kizayuni Israel na kuiunga mkono Palestina
Apr 26, 2019 08:01Sambamba na kusherehekea mwaka wa 74 wa kuwa huru nchi ya Italia na utawala wa Kifashisti, raia wa nchi hiyo mjini Roma, mji mkuu wa Italia wamefanya maandamano kuliunga mkono taifa madhlumu la Palestina.
-
Wakuu wa Baraza la Mpito la Kijeshi la Sudan wajiuzulu
Apr 25, 2019 07:47Viongozi watatu kati ya 10 wa Baraza la Mpito la Kijeshi la Sudan wametangaza kujiuzulu, huku wananchi wa nchi hiyo wakitazamiwa kuendelea na maandamano yao leo Alkhamisi, kulishinikiza jeshi likabidhi madaraka kwa raia.
-
Waandamanaji Sudan kutangaza Baraza la Mpito la Kiraia
Apr 21, 2019 14:15Chama cha Wanataaluma Sudan kimetangaza kuwa kinajiandaa kutangaza Baraza la Mpito la Kiraia, litakalochukua madaraka kutokana kwa Baraza la Mpito la Kijeshi la nchi hiyo.
-
Walibya waandamana kulaani hatua ya Trump kumpigia simu Jenerali Haftar
Apr 20, 2019 13:07Wananchi wa Libya wamefanya maandamano mjini Tripoli kukosoa hatua ya Rais Donald Trump kumpigia simu jenerali muasi Khalifa Haftar mwenye makao yake katika mji wa Benghazi, magharibi mwa Libya, na ambaye amekuwa akiendesha kampeni ya kijeshi ya kutaka kuuteka mji mkuu Tripoli.
-
Polisi: Watu 16 wameuawa kwa risasi katika maandamano nchini Sudan
Apr 13, 2019 08:09Polisi nchini Sudan imesema kuwa, kwa akali watu 16 wameuawa huku wengine zaidi ya 20 wakijeruhiwa katika maandamano ya Alkhamisi na jana Ijumaa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum.
-
Jenerali aliyemrithi Omar al-Bashir ajiuzulu pia, maandamano yashtadi Sudan
Apr 13, 2019 04:07Jenerali Awad Mohamed Ahmad Ibn Auf, Waziri wa Ulinzi wa Sudan aliyetangazwa kuwa Kaimu Rais baada ya Omar al-Bashir kung'olewa madarakani naye ametangaza kujiuzulu, baada ya makumi ya maelfu ya Wasudani kuendeleza maandamano wakitaka makabidhiano ya kiraia ya uongozi.
-
Wairani waandamana kote nchini kuliunga mkono Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH)
Apr 12, 2019 15:15Wananchi wa Iran katika kila kona ya nchi wamemiminika mabarabarani kushiriki maandamano ya kuonyesha uungaji mkono wao kwa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Waalgeria washadidisha maandamano baada ya kuteuliwa rais wa mpito
Apr 09, 2019 14:41Maelfu ya wananchi wa Algeria wakiwemo wanafunzi wa Vyuo Vikuu wamemiminika mabarabarani kushiriki maandamano ya kupinga kuteuliwa rais wa mpito wa nchi hiyo.
-
Wizara: Israel inatumia gesi za sumu dhidi ya waandamanaji wa Kipalestina
Apr 09, 2019 14:38Msemaji wa Wizara ya Afya ya Gaza amesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekuwa ukitumia gesi za sumu dhidi ya waandamanaji wa Kipalestina katika ukanda huo.