Jan 25, 2023 03:03
Wilaya kadhaa katika mkoa wa Mahajanga kaskazini magharibi mwa Madagascar zimekumbwa na mafuriko pamoja na barabara zinazoziunganisha wilaya hizo kueleke amji mkuu, Antananarivo. Kimbunga kwa jina la "Cheneso" kinaendelea kukiathiri kisiwa hicho kinachopatikana katika bahari ya Hindi huku watu zaidi ya 15,000 pia wakiathirika.