Misikiti minne ya Jamia nchini Uholanzi inatazamiwa kufungwa kutokana na kushadidi chuki dhidi ya Waislamu, siku mbili baada ya shambulizi la kikatili dhidi ya msikiti na kituo cha kidini mjini Quebec nchini Canada.
Baada ya kuongezeka hisia za chuki na uadui dhidi ya Waislamu huko Amerika Kaskazini hususan baada ya kuingia madarakani Rais Donald Trump nchini Marekani, hivi sasa matokeo mabaya ya jambo hilo yameanza kuonekana.
Kwa akali watu watano wameuawa katika hujuma ya kikatili dhidi ya msikiti mmoja katika mji wa Quebec nchini Canada usiku wa kuamkia leo.
Katika muendelezo wa sera za chuki dhidi ya Uislamu na hujuma zinazolenga misikiti nchini Marekani, vyombo vya usalama vya nchi hiyo vimeripoti kuwa msikiti mwingine mmoja umechomwa moto katika jimbo la Texas.
Baraza la Sharia la Waislamu wa Afrika Kusini (MJC) limelaani kitendo cha chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu kilichofanywa kwenye msikiti wa mji wa Simon katika jimbo la Cape Town cha kuweka pua ya nguruwe na kumwaga damu kwenye mlango wa msikiti huo.
Kikosi cha Kupambana na Ugaidi cha Jeshi la Polisi nchini Uganda (JATT) jana Jumanne asubuhi kilifanya msako mkali katika msikiti wa Nakasero ulioko katika barabara ya Snay bin Amin jijini Kampala na kukamata watu kadhaa wakiwemo walinzi wa msikiti huo.
Watu watatu wamejeruhiwa baada ya mtu aliyekuwa na bunduki kushambulia msikiti na kufyatua risasi ovyo akiwalenga waumini waliokuwa wakitekeleza ibada zao katika mji wa Zurich nchini Uswisi usiku wa kuamkia leo.
Zaidi ya ya vituo vya Kiislamu na misikiti 100 imehujumiwa nchini Uingereza katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Vitendo vya chuki dhidi ya Waislamu na maeneo yao ya ibada vimezidi kuongezeka nchini Marekani, na habari za karibuni kabisa zinasema kuwa gaidi mmoja ametoa ametoa matamshi ya vitisho dhidi ya misikiti nchini humo.
Watu wasiopungua 23 wameuawa na makumi ya wengine wamejeruhiwa katika shambulio la kigaidi lililofanywa ndani ya msikiti katika Sala ya Ijumaa wilayani Mohmand nchini Pakistan.