-
Vikosi vya jeshi la Marekani vyakiri kuua raia 33 wa Afghanistan
Jan 12, 2017 15:28Vikosi vya jeshi la Marekani vilivyoko chini ya mwavuli wa shirika la kijeshi la NATO vimekiri kuwa viliua raia 33 wa Afghanistan wakiwemo watoto wadogo katika shambulio la mwezi Novemba jana lililofanywa kwa kisingizio cha kupambana na wanamgambo wa kundi la Taliban.
-
Russia yaikosoa vikali Nato kwa kuanzisha mgogoro
Jul 13, 2016 07:22Maria Zakharova Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia jana Jumanne aliwasilisha taarifa na kueleza kuwa Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (Nato) una nafasi kubwa katika kuzua migogoro na kuendeleza hali ya mivutano katika maeneo mbalimbali duniani.
-
NATO yaanza mazoezi ya kijeshi baharini karibu na Russia
Jul 12, 2016 03:45Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO) umeanza mazoezi ya kijeshi karibu kabisa na Russia.
-
Radiamali ya Iran kwa matamshi ya Nato kuhusu mpango wake wa makombora
Jul 11, 2016 07:46Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameitaja taarifa ya mwisho ya kikao cha wakuu wa Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (Nato) kuhusu mpango wa makombora wa Iran kuwa ni madai ya kukaririwa na yasiyo na msingi.
-
Russia yalaani NATO kujipania kuelekea Mashariki
Jul 10, 2016 14:37Russia imelaani vikali hatua ya muungano wa kijeshi wa NATO kujipanua na kuelekeza nguvu zake Moscow wakati ambapo hakuna tishio lolote kutoka mashariki.
-
Tetesi za kuingia kwa mara nyingine NATO nchini Libya
May 26, 2016 06:57Sambamba na kuongezeka matatizo ya kiusalama Libya, kuna taarifa kuwa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO linapanga kuingilia tena kijeshi katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Ombi la NATO la kustawisha ushirikiano na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na (P)GCC
Apr 10, 2016 07:10Naibu Katibu Mkuu wa Shirika la Kijeshi la NATO, Alexander Vershbow ametaka kustawishwa ushrikiano kati ya shirika hilo la kijeshi na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (P)GCC pamoja na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.
-
Nato na Russia huenda zikaanzisha mazungumzo baada ya miaka miwili
Apr 08, 2016 14:06Russia imesema kuwa huenda ikafanya mazungumzo na Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi Nato katika wiki chache zijazo.
-
NATO kupanua operesheni za kukabiliana na wakimbizi
Mar 07, 2016 16:16Katibu Mkuu wa shirika la kijeshi la NATO, Jens Stoltenberg amesema kuwa jumuiya hiyo itapanua zaidi operesheni zake katika maji ya karibu na nchi za Ugiriki na Uturuki ili kuzuia wimbi la wahamiaji haramu kuelekea katika nchi za Magharibi.
-
Wanachama wa NATO kutoingilia vita vya Uturuki,Russia
Feb 21, 2016 02:49Baadhi ya nchi wanachama wa Shirika la Kijeshi la NATO zimetahadharisha kuhusu kushtadi kwa mivutano baina ya Uturuki na Russia na kusisitiza kuwa hazitoingilia endapo vitazuka vita baina ya nchi hizo mbili.