-
Nyumba elfu moja zaharibiwa na mafuriko nchini Nigeria
Jun 04, 2017 23:55Mratibu wa huduma za dharura wa shirika la kimataifa la wahajiri amesema kuwa, nyumba zisizopungua elfu moja zimeharibiwa na mafuriko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
UN yatahadharisha kuhusu kusimamishwa misaada ya kibinadamu nchini Nigeria
May 25, 2017 23:24Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa, kupunguzwa bajeti za umoja huo kumezikwamisha taasisi zake katika kuendesha miradi mbalimbali ya kimataifa ikiwa ni pamoja na kuwatumia chakula waathirika wa mashambulizi ya kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Polisi Nigeria yatumia mabavu kuzima maandamano ya Waislamu
May 23, 2017 02:39Kwa mara nyingine tena polisi nchini Nigeria imetumia mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwasha kutawanya maandamano ya wananchama wa Harakati ya Kiislamu nchini humo wanaoshinikiza kuachiwa huru kiongozi wao, Sheikh Ibrahim Zakzaky.
-
Jeshi la Nigeria laua wanachama 13 wa Boko Haram eneo la Ziwa Chad
May 21, 2017 09:09Kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limeendelea kupata pigo kutoka kwa askari wa jeshi la Nigeria, ambapo wanachama 13 wa genge hilo wameuawa kwenye makabaliano mapya yaliyotokea jana katika eneo la Ziwa Chad.
-
Watu sita wauawa katika shambulio la Boko Haram katika mji wa Maiduguri
May 15, 2017 23:23Watu wasiopungua 6 wanaripotiwa kuuawa kufuatia shambulio la kundi la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Idadi ya walioaga dunia kutokana na homa ya uti wa mgongo Nigeria yapindukia elfu moja
May 11, 2017 10:27Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Nigeria NCDC kimesema idadi ya watu walioaga dunia kufikia sasa kutokana na homa ya uti wa mgongo ni zaidi ya elfu moja.
-
Rais Buhari wa Nigeria arejea London, Uingereza kwa matibabu
May 08, 2017 02:23Muda mfupi baada ya kuonana na wanafunzi wa kike 82 waliokuwa wamewatekwa nyara na kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram katika mji wa Chibok mwaka 2014, mkabala wa kuachiwa huru wafungwa wa kundi hilo, Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria ameondoka nchini na kwenda Uingereza kwa ajili ya kile kinachosemwa ni uchunguzi wa kiafya.
-
Watu 26 waaga dunia baada ya mabasi 2 kugongana Nigeria
May 07, 2017 08:47Kwa akali watu 26 wamepoteza maisha katika ajali mbaya ya barabarani katika mji wa Lagos magharibi mwa Nigeria.
-
Wasichana 82 waachiliwa huru na Boko Haram Nigeria kwa kubadilishana na wafungwa wa kundi hilo
May 06, 2017 22:41Ofisi ya Rais wa Nigeria imetangaza kuwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram limewaachia huru wanafunzi wa kike 82 miongoni mwa wasichana zaidi ya 200 waliokuwa wamewateka nyara katika mji wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo wa Chibok mwaka 2014, mkabala wa kuachiwa huru wafungwa wa kundi hilo.
-
Maafisa wawili wa serikali Nigeria wahukumiwa kifungo jela kwa kuuza magunia ya misaada ya chakula
May 05, 2017 03:25Maafisa wawili wa serikali ya Nigeria wamehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kila mmoja kwa kuchukua na kuuza magunia ya mchele yapatayo c300 ya misaada kwa ajili ya watu waliohama makwao kwa sababu ya mapigano na uhaba wa chakula.