-
Wapalestina 3 wauawa shahidi na jeshi la Israel Ukanda wa Gaza
Jan 22, 2020 08:28Wanajeshi katili wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi kwa kuwapiga risasi Wapalestina watatu katika uzio wa Ukanda wa Gaza.
-
Maaskofu wa Kikatoliki wataka kutambuliwa rasmi nchi huru ya Palestina
Jan 19, 2020 07:56Maaskofu wa Ulaya, America ya Kaskazini na Afrika Kusini amezitaka nchi zao kuitambua rasmi nchi huru ya Palestina na kusisitiza udharura wa kuwapa Wapalestina haki zao zote.
-
Liverpool FC yawatetea Wapalestina, yakataa udhamini wa Puma kutokana na ushirikiano wake na Israel
Jan 14, 2020 03:20Klabu ya soka ya Uingereza, Liverpool imekataa ufadhili wa kifedha wa kampuni ya Puma ikipinga ushirikiano wa kampuni hiyo na utawala haramu wa Israel. Liverpool imechukua hatua hiyo kutokana na mashinikizo ya mashabiki wa klabu hiyo wanaopinga mauaji na ukatili unaofanywa na Israel dhidi ya raia wasio na hatia wa Palestina.
-
Ripoti: Israel iliwateka nyara Wapalestina 5,500 mwaka 2019
Jan 01, 2020 04:33Shirika moja la kutetea haki za wafungwa limefichua kuwa, kwa akali Wapalestina 5,500 walitekwa nyara au kutiwa mbaroni na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel mwaka uliomalizika wa 2019.
-
Hamas yakataa mapatano ya aina yoyote na utawala wa Kizayuni
Dec 29, 2019 04:35Mwakilishi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amepinga kufikiwa mapatatano yoyote kati ya harakati hiyo na utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kutoa suhula mbalimbali huko Ghaza mkabala na Hamas kusitisha uvurumishaji wa makombora katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Israel yatishia kuwaua kigaidi viongozi wa Palestina
Dec 27, 2019 21:01Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa mara nyingine ametishia kuwaua kigaidi viongozi wa Palestina.
-
Kuendelea utata kuhusu kufanyika uchaguzi wa Palestina
Dec 27, 2019 06:49Baada ya kupita zaidi ya miezi mitatu tokea Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) atangaze azma ya kufanyika uchaguzi, bado kunaendelea kushuhudiwa utata na hitilafu kuhusu kadhia hiyo.
-
Hamas: Utawala wa Kizayuni ndio utakaobeba dhima ya lolote litakalotokea + Video
Dec 26, 2019 08:23Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kuwa, utawala wa Kizayuni ndio utakaobeba dhima ya lolote litakalotokea kutokana na mashambulizi yake ya mara kwa mara katika Ukanda wa Ghaza.
-
UN yatiwa wasiwasi na ujenzi wa vitongoji vya walowezi katika ardhi ya Palestina
Dec 24, 2019 04:30Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika Mashariki ya Kati amesema kuwa, mwenendo wa ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika eneo la Ukingo wa Magharibi na Quds Mashariki huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu umeongezeka kwa asilimia 70 mwaka huu ikilinganishwa na mwaka wa kabla yake.
-
Waziri wa Israel aitaka Tel Aviv kubomoa kijiji kimoja cha Wapelestina kila siku
Dec 22, 2019 23:13Waziri wa Usafirishaji wa Israel ametoa wito wa kuvunjwa kijiji kimoja cha Palestina kila siku na kuangamiza kabisa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ikiwa ni katika kulipiza kisasi dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wa kuanza uchunguzi kuhusu jinai zilizofanywa na utawala wa Israel katika Ukingo wa Magharibi ikiwemo Quds na Ukanda wa Gaza.