-
Wapalestina zaidi ya 8,500 wametiwa nguvuni Ukingo wa Magharibi tangu Oktoba 7 hadi sasa
Apr 29, 2024 23:16Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina imetangaza katika ripoti yake kwamba utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel umewatia nguvuni Wapalestina 8,505 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan tangu tarehe 7 Oktoba 2023 mara baada ya kutekelezwa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Mgombea wa uchaguzi wa rais Marekani atiwa nguvuni katika maandamano ya watetezi wa Palestina
Apr 28, 2024 23:06Polisi nchini Marekani imemtia nguvuni mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu nchini humo ambaye alikuwa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Washington.
-
HAMAS: Msaada mpya wa Marekani kwa Israel ni kwa ajili ya kuendeleza mauaji ya umati
Apr 21, 2024 23:03Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeilaani Marekani kwa kupasisha msaada mwingine kwa utawala wa Kizayuni na kusema kuwa msaada huo ni kwa ajili ya kuendeleza mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Marekani; kizuizi kikuu kwa Palestina kuwa mwanachama kamili katika Umoja wa Mataifa
Apr 20, 2024 08:47Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu wa Israel kwa mara nyingine imetumia kura ya turufu (Veto) na kuzuia kupasishwa uanachama kamili wa Palestina ndani ya Umoja wa Mataifa.
-
Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN
Apr 20, 2024 03:13Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
-
OIC yalaani hatua ya Marekani kuzuia azma ya Palestina kuwa mwanachama kamili wa UN
Apr 19, 2024 23:29Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani hatua ya Marekani ya kuzuia ombi la Palestina la kutaka uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa msaada wa baadhi ya nchi za Magharibi hususan Marekani.
-
Kupingwa njama za Netanyahu za kutaka kususiwa shughuli za UNRWA ndani ya Baraza la Usalama
Apr 19, 2024 11:57Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya kikao kujadili shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) kufutia maombi ya Algeria na Jordan.
-
Marekani yalipigia kura ya veto azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili wa Umoja wa Mataifa
Apr 19, 2024 03:59Marekani, ambayo ni muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imeendeleza sera yake ya kudhoofisha kupatikana haki za Wapalestina kwa kutumia vibaya haki yake ya kura ya turufu na kukwamisha azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
-
Mkuu wa UNRWA alaumu vikali hila ya Israel ya kutaka shirika hilo la kusaidia Wapalestina livunjwe
Apr 18, 2024 02:51Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kuwasaidia Wapalestina, UNRWA, Philippe Lazzarini amelaumu vikali kampeni ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kulisambaratisha shirika hilo.
-
Marekani inawashinikiza kwa siri wanachama wa UNSC wapinge Palestina kuwa mwanachama kamili wa UN
Apr 18, 2024 02:51Marekani inazishinikiza kwa siri nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kukataa ombi la Palestina kuwa mwanachama kamili wa taasisi hiyo kuu ya kimataifa.