Trump aapa "kutimua wanafunzi" na kukandamiza wanaounga mkono Palestina akichagualiwa tena kuwa rais
Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump ameapa kuwa atakandamiza maandamano ya watetezi na waungaji mkono wa Palestina yanayoendelea kufanywa katika vyuo vikuu vya nchi hiyo na kusisitiza kuwa "atawafukuza" wanafunzi wanaohudhuria maandamano hayo, ikiwa atachaguliwa kurudi tena madarakani.
Katika miezi ya hivi karibuni, maandamano ya kupinga jinai za kinyama za mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza yametikisa taasisi mbalimbali za elimu katika kila pembe ya Marekani. Harakati hizo zilianzia Chuo Kikuu cha Columbia mjini New York, ambapo uwekaji mahema na kupiga kambi kwenye viwanja vya vyuo kulivuruga shughuli za masomo katika wiki za mwisho na kupelekea hata kuakhirishwa mahafali za kuhitimu masomo.
Kwa mujibu wa gazeti la The Washington Post, wafadhili wa chama cha Republican wamemtaka Trump achukue msimamo mkali zaidi wa kuiunga mkono Israel na waziri mkuu wake Benjamin Netanyahu.
Trump pia ameripotiwa kuwaambia wafadhili hao katika faragha kwamba anaunga mkono haki ya utawala huo wa Kizayuni ya kuendeleza mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Ghaza.../