-
Rais wa Russia akutana na Rais wa Syria na kumpongeza kufuatia mafanikio dhidi ya magaidi
Nov 21, 2017 04:38Rais Vladimir Putin wa Russia amempongeza Rais Bashar al-Assad wa Syria kufuatia ushindi mkubwa wa jeshi la Syria dhidi ya magaidi.
-
Russia yawaonya raia wake kutotembelea Ulaya na Marekani
Nov 18, 2017 11:50Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imewatahadharisha raia wake walio na nia ya kutembelea Marekani na nchi za Ulaya katika kipindi cha sherehe za mwaka mpya wa Milaadia na kusema kuwa kuna hatari ya kutokea mashambulizi ya kigaidi katika nchi hizo.
-
Russia: Marekani ni dola vamizi, halikualikwa nchini Syria
Nov 17, 2017 00:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa kuwepo wanajeshi wa Marekani katika ardhi ya Syria ni uvamizi na ni kinyume cha sheria.
-
Russia: Uchunguzi ufanyike kuhusu shambulizi la anga la Marekani Kunduz, Afghanistan
Nov 12, 2017 01:04Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imewataka maafisa wa serikali ya Afghanistan na taasisi za kimaraifa za kutetea haki za binadamu wafanye uchunguzi kamili na usiopendelea upande wowote kuhusu shambulizi la anga la Marekani katika mji wa Kunduz nchini Afghanistan.
-
Marais Putin na Macron: Kupitia upya makubaliano ya JCPOA ni jambo lisilokubalika
Nov 03, 2017 01:02Rais Vladmir Putin wa Russia na Emmanuel Macron wa Ufaransa wamesema kuwa, kuangaliwa upya makubaliano ya nyuklia ya Iran JCPOA, ni jambo lisilokubalika.
-
Rais Putin wa Russia atarajiwa Iran kuhudhuria mkutano wa pande tatu
Nov 01, 2017 01:01Rais Vladimir Putin wa Russia na Rais Ilham Aliyev wa Jamhuri ya Azerbaijan leo Jumatano wanatarajiwa kuwasili mjini Tehran kwa ajili ya mkutano wa pande tatu na Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kutekelezwa vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia
Oct 28, 2017 23:38Serikali ya Marekani imechapisha orodha ya makampuni ya Russia iliyoyawekea vikwazo baada ya kuchapisha sheria mpya ya vikwazo dhidi ya Russia. Katika uwanja huo Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani imechapisha orodha inayobainsha sheria hiyo ya vikwazo kuhusu Iran, Korea ya kaskazini na Russia na kutangaza kuyawekea vikwazo makampuni 39 ya kiulinzi na kiitelijinsia ya Russia.
-
Korea Kaskazini: Marekani ndio iliyoanzisha mchezo wa nyuklia, tutakabiliana nayo
Oct 21, 2017 12:57Afisa wa ngazi ya juu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini amesema kuwa, Pyongyang itaendelea kujiimarisha zaidi kwa silaha za nyuklia kwa ajili ya kukabiliana na vitisho vya Marekani.
-
Marekani yakiri magaidi wanatumia silaha za kemikali Syria
Oct 20, 2017 22:58Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kwa mara ya kwanza imekiri kwamba, magaidi wanatumia silaha za kemikali huko Syria.
-
Maghala kadhaa makubwa ya silaha za Marekani na Israel yagunduliwa katika maficho ya Daesh Syria
Oct 15, 2017 10:48Maghala kadhaa makubwa ya silaha za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel yamegunduliwa katika maficho ya genge la kigaidi la Daesh (ISIS) katika mji uliokombolewa wa al Mayadin mkoani Dayr al-Zawr, mashariki mwa Syria.