-
Miripuko pacha yatikisa Somalia, kadhaa wapoteza maisha
Jun 21, 2023 12:14Watu kadhaa wanahofiwa kuuawa katika mashambulizi pacha ya mabomu katika mji wa Bardhere ulioko katika eneo la Gedo, kusini magharibi mwa Somalia.
-
Mapigano juu ya mageuzi ya katiba yaua watu 9 Puntland, Somalia
Jun 21, 2023 03:43Watu wasiopungua tisa wameuawa katika mapigano yaliyosababishwa na suala tata la kuifanyia marekebisho katiba katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia.
-
Magaidi 19 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab waangamizwa Somalia
Jun 12, 2023 11:16Wanachama wasiopungua 19 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameangamizwa kufuatia operesheni ya jeshi la Somalia katika eneo la kusini la Lower Shabelle.
-
Waliouawa katika miripuko ya mabomu Somalia wakaribia 30
Jun 10, 2023 10:04Idadi ya watu walioaga dunia kutokana na miripuko ya mabomu katika eneo la Lower Shabelle nchini Somalia imeongezeka na kufikia watu 27.
-
UN: Mapigano yasimamishwe mara moja nchini Somalia
Jun 08, 2023 07:20Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetoa wito kwa pande zinazozozana kutia saini makubaliano ya kusitisha mapigano nchini Somalia likisisitiza udharura wa kuheshimiwa kikamilifu mamlaka, uhuru wa kisiasa na umoja wa ardhi ya Somalia.
-
Museveni: Wanajeshi 54 wa Uganda wameuawa na al-Shabaab Somalia
Jun 04, 2023 11:32Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema makumi ya askari wa Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo (UPDF) waliuawa katika shambulio la wanamgambo wa al-Shabaab nchini Somalia wiki iliyopita.
-
17 wauawa katika mapigano baina ya al-Shabaab na jeshi la Somalia
May 30, 2023 16:18Kwa akali watu 17 wameuawa baada ya wanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabaab kushambulia kambi ya jeshi katika mji wa Masagawa, katikati ya Somalia.
-
Somalia kuanzisha upigaji kura wa moja kwa moja wa wananchi mwaka 2024
May 28, 2023 11:06Somalia imetangaza kuwa itaanzisha mfumo wa upigaji kura wa moja kwa moja wa wananchi. Hatua hii inafuatia ahadi ya Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia mwezi Machi mwaka huu ya kukomesha mfumo tata wa upigaji kura usio wa moja kwa moja unaoendelea tangu mwaka 1969.
-
Museveni: Tutalipiza kisasi cha shambulio la al-Shabaab dhidi ya UPDF Somalia
May 28, 2023 06:54Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo UPDF litatoa jibu kali kufuatia shambulizi la wanamgambo wa al-Shabaab dhidi ya askari walinda amani wa Uganda walioko nchini Somalia.
-
UN: Zaidi ya watu milioni moja wamekimbia makazi yao katika muda wa miezi minne Somalia
May 25, 2023 01:27Wasomali zaidi ya milioni moja wamekuwa wakimbizi nchini humo katika kipindi cha zaidi ya miezi minne kutokana na ukame, mashambulizi ya wanamgambo wa al Shabaab na mafuriko. Haya yameelezwa na taasisi za misaada ya kibinadamu.