Vikosi Maalumu vya Danab vya jeshi la Somalia vimeua makumi ya magaidi wa al-Shabaab katika operesheni ya hivi punde katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amesema lengo la operesheni za kijeshi zinazoendelea nchini humo ni kulitokomeza na kulisambaratisha kundi la kigaidi la al-Shabaab katika kipindi cha miezi mitano ijayo.
Jeshi la Somalia limetangaza kuwa limewaangamiza wanachama wapatao 20 wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab katika mkoa wa Lower Shabelle kusini mwa nchi hiyo.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema limeongeza hatua za dharura ili kuokoa maisha na kuzuia maambukizi zaidi ya kipindupindu nchini Somalia baada ya watu 30 kufariki dunia kutokana na ugonjwa huo tangu Januari mwaka huu.
Wanajeshi kadhaa wa Somalia wamepoteza maisha baada ya gari lililokuwa limewabeba kukanyaga bomu katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
Wanachama 25 wa kundi la kigaidi la al-Shabab la Somalia wameangamizwa akiwemo mmoja wa makamanda wao wa ngazi za juu.
Wanachama wasiopungua 60 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameuawa katika operesheni ya pamoja ya jeshi la Somalia na vikosi vya kigeni kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Wanachama wasiopungua 100 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameripotiwa kuuawa katika operesheni ya pamoja ya jeshi la Somalia na vikosi vya kigeni katikati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Viongozi wa Somalia wametangaza kuwa, magaidi 20 wa kundi la wanamgambo wa al-Shabab wameuawa na vikosi vya serikali katikati mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Miripuko miwili ya mabomu iliyotokea Mogadishu, mji mkuu wa Somalia, imesababisha watu kadhaa kuuawa na kujeruhiwa.