-
Somalia: Israel kuwahamishia kwa nguvu Wapalestina Somaliland ni kinyume cha sheria za kimataifa
Jan 11, 2026 03:26Waziri wa Ulinzi wa Somalia, Ahmed Moalim Fiqi, ameishutumu Israel kwa kupanga kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Gaza na kuwapeleka katika eneo lililojitenga la Somaliland, akiukashifu mpango huo alioutaja kuwa ni "ukiukaji mkubwa" wa sheria za kimataifa.
-
Somalia yakanusha madai ya Marekani ya kutwaa chakula cha WFP
Jan 08, 2026 22:53Somalia jana Alhamisi ilikanusha madai ya Marekani kwamba maafisa wa eneo hilo wametwaa bidhaa za chakula kutoka katika ghala la shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), huku Washington ikisimamisha misaada kwa Mogadishu kusubiri uchunguzi.
-
Somalia yapokezwa uenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama la UN
Jan 03, 2026 02:33Somalia jana Ijumaa ilichukua urais wa zamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha mwezi huu wa Januari, ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kushikilia wadhifa huo tangu ilipohudumu mara ya mwisho katika baraza hilo mwaka 1971-72.
-
Jeshi la Somalia laangamiza makumi ya magaidi wa al-Shabaab
Jan 01, 2026 23:17Makumi ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabaab lenye misimamo ya kufurutu ada , wameangamizwa katika operesheni ya wanajeshi wa Somalia.
-
Somaliland yajitoa kimasomaso, yakanusha kuafiki kujengwa kambi za kijeshi za Israel
Jan 01, 2026 23:16Eneo la Somaliland la kaskazini mwa Somalia limekanusha madai kwamba lilikubali kuwa mwenyeji wa vituo vya kijeshi vya Israel na kuwapokea Wapalestina waliofurushwa kutoka Gaza ili kutambuliwa na Israel.
-
Rais wa Somalia: Somaliland inashirikiana na Israel dhidi ya Wapalestina
Dec 31, 2025 22:56Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amezinukuu ripoti za kiitelijinsia na kusema kuwa eneo lililojitenga la na nchi hiyo la Somaliland limekubali kuwapokea Wapalestina na kuanzishwa kambi ya kijeshi ya Israel katika eneo hilo mkabala wa kutambuliwa rasmi na Israel.
-
Maandamano ya kuilaani Israel kwa 'kuitambua Somaliland' yaenea kote Somalia
Dec 30, 2025 22:56Maelfu ya wananchi wa Somalia wameendelea kumiminika mabarabarani katika miji mbali mbali ya nchi hiyo, kupinga na kulaani uamuzi wa utawala haramu wa Israel wa kulitambua eneo la Somaliland la kaskazini mwa nchi kama taifa huru.
-
Somaliland katika kitovu cha kuzingatiwa kijiopilitiki; Je Israel inataka kutia mguu katika Lango Bahari la Bab al-Mandab?
Dec 30, 2025 22:53Mataifa na asasi mbalimbali za Kiafrika, Kiarabu na Kiislamu zimepinga vikali hatua ya utawala vamizi wa Israel ya kulitambua rasmi eneo la 'Somaliland', ambalo limejitenga na Somalia, kama taifa huru na lenye mamlaka kamili, hatua ambayo imekabiliwa na radiamali kali ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na jamii ya kimataifa.
-
EAC yaunga mkono mamlaka ya kujitawala Somalia baada ya Israel kuitambua rasmi Somaliland
Dec 29, 2025 06:26Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imevunja ukimya wake kuhusu hali ya mvutano unaoendelea nchini Somalia na Somaliland, na kuthibitisha uungaji mkono wake kwa Somalia.
-
Wasomali waandamana kuilaani Israel kwa kuitambua Somaliland
Dec 29, 2025 06:20Mamia ya wanachi wa Somalia jana Jumapili walifanya maandamano katika mji mkuu wa nchi hyo, Mogadishu kupinga na kulaani uamuzi wa utawala haramu wa Israel wa kuitambua kana nchi huru Somaliland, eneo la kaskazini mwa Somalia ambalo lilijitangazia uhuru wake mwaka 1991.