-
Magaidi 87 wa al Shabab wauawa kusini mwa Somalia
Jul 24, 2018 11:41Serikali ya Somalia imetangaza kuwa imewaangamiza magaidi 87 wa kundi la al Shabab katika mapigano yaliyotokea jana kusini mwa nchi hiyo.
-
Kundi la al Shabab lashambulia kambi ya jeshi na kuuwa wanajeshi 27 Somalia
Jul 23, 2018 03:38Kundi la wanamgambo wa al Shabab lenye makao yake nchini Somalia limetangaza hii leo kuwa limeshambulia kambi moja ya jeshi kwa kulipua bomu lililotegwa garini huko kusini mwa nchi hiyo na kuuwa wanajeshi 27.
-
Al-Shabaab yateka mji muhimu katika eneo la Puntland, Somalia
Jul 20, 2018 09:48Kundi la kigaidi na ukufurishaji la al-Shabaab la Somalia limeteka mji mdogo lakini wa kistratajia ulioko karibu na eneo la milima ya Galgala, kusini mwa jiji la Bosaso katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland.
-
Mripuko wa bomu watokea karibu na ikulu ya rais wa Somalia
Jul 07, 2018 09:55Polisi ya Somalia imetangaza habari ya kutokea mripuko wa bomu karibu na ikulu ya Rais Mohamed Abdullahi Mohamed wa nchi hiyo mjini Mogadishu.
-
EU yaishambulia Imarati kwa kuvuruga uthabiti Somalia
Jul 06, 2018 08:57Bunge la Umoja wa Ulaya limezikosoa vikali Umoja wa Falme za Kiarabu na Saudi Arabia kwa kuikatia Somalia misaada kutokana na nchi hiyo ya Pembe ya Afrika kutangaza msimamo wa kutoegemea upande wowote katika mgogoro kati ya nchi nne za Kiarabu zikiongozwa na Saudia kwa upande mmoja na Qatar kwa upande wa pili.
-
Wanafunzi wa Kiafrika wanaotuhumiwa kwa ugaidi wakamatwa Uturuki
Jul 01, 2018 22:07Makumi ya wanafunzi wa Kiafrika hususan raia wa Somalia wamekamatwa nchini Uturuki, wakihusishwa na Shirika la Kigaidi la Fathullah FETO, linalodaiwa kuratibu na kutekeleza jaribio la mapinduzi lililofeli la mwaka 2016.
-
Magaidi 7 wa Al Shabab, akiwemo Mtanzania, waangamizwa katika mapigano Somalia
Jun 26, 2018 03:14Jeshi la Somalia limewaangamiza magaidi saba wa kundi la kigaidi la Al Shabab katika mapigano yaliyojiri katika eneo la Lower Juba kusini mwa nchi hiyo.
-
Mabaharia 17 wa Kiirani waliokamatwa Somalia waachiwa huru
Jun 21, 2018 09:11Mabaharia 17 wa Kiirani waliokuwa wameingia kimakosa katika maji ya Somalia na kutiwa nguvuni mwishoni mwa mwaka jana 2017 wameachiwa huru na kurejea nchini.
-
Kimbunga cha Kitropiki kimeua watu 53 Somalia
Jun 15, 2018 10:45Shirika la Kuratibu Misaada ya Kibinadamu la Umoja wa Mataifa (OCHA) limesema watu wasiopungua 53 wamefariki dunia Somalia kufuatia kimbunga cha kitropiki kilichoikumba nchi hiyo hivi karibuni.
-
Watu 7 wafa maji katika ajali ya boti kusini mwa Somalia
Jun 12, 2018 22:11Watu saba wamethibitishwa kupoteza maisha baada ya boti yao kuzama katika Mto Shabelle, kusini mwa Somalia.