-
EU yaishambulia Imarati kwa kuvuruga uthabiti Somalia
Jul 06, 2018 08:57Bunge la Umoja wa Ulaya limezikosoa vikali Umoja wa Falme za Kiarabu na Saudi Arabia kwa kuikatia Somalia misaada kutokana na nchi hiyo ya Pembe ya Afrika kutangaza msimamo wa kutoegemea upande wowote katika mgogoro kati ya nchi nne za Kiarabu zikiongozwa na Saudia kwa upande mmoja na Qatar kwa upande wa pili.
-
Wanafunzi wa Kiafrika wanaotuhumiwa kwa ugaidi wakamatwa Uturuki
Jul 01, 2018 22:07Makumi ya wanafunzi wa Kiafrika hususan raia wa Somalia wamekamatwa nchini Uturuki, wakihusishwa na Shirika la Kigaidi la Fathullah FETO, linalodaiwa kuratibu na kutekeleza jaribio la mapinduzi lililofeli la mwaka 2016.
-
Magaidi 7 wa Al Shabab, akiwemo Mtanzania, waangamizwa katika mapigano Somalia
Jun 26, 2018 03:14Jeshi la Somalia limewaangamiza magaidi saba wa kundi la kigaidi la Al Shabab katika mapigano yaliyojiri katika eneo la Lower Juba kusini mwa nchi hiyo.
-
Mabaharia 17 wa Kiirani waliokamatwa Somalia waachiwa huru
Jun 21, 2018 09:11Mabaharia 17 wa Kiirani waliokuwa wameingia kimakosa katika maji ya Somalia na kutiwa nguvuni mwishoni mwa mwaka jana 2017 wameachiwa huru na kurejea nchini.
-
Kimbunga cha Kitropiki kimeua watu 53 Somalia
Jun 15, 2018 10:45Shirika la Kuratibu Misaada ya Kibinadamu la Umoja wa Mataifa (OCHA) limesema watu wasiopungua 53 wamefariki dunia Somalia kufuatia kimbunga cha kitropiki kilichoikumba nchi hiyo hivi karibuni.
-
Watu 7 wafa maji katika ajali ya boti kusini mwa Somalia
Jun 12, 2018 22:11Watu saba wamethibitishwa kupoteza maisha baada ya boti yao kuzama katika Mto Shabelle, kusini mwa Somalia.
-
Magaidi wa al Shabab wajeruhi watu saba kusini mwa Somalia
Jun 10, 2018 03:25Afisa mmoja wa jeshi la Somalia ametangaza habari ya kujeruhiwa watu saba katika shambulio la kujiripua kwa mabomu lililofanywa na gaidi mmoja wa al Shabab katika kambi moja ya kijeshi iliyoko kusini mwa nchi hiyo, usiku wa kuamkia leo.
-
Askari 5 wa Marekani wauawa na kujeruhiwa na al-Shabaab Somalia
Jun 09, 2018 03:35Askari mmoja wa Marekani ameuawa huku wengine wanne wakijeruhiwa katika operesheni ya pamoja ya vikosi vya US na askari wa Umoja wa Afrika dhidi ya ngome ya wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab nchini Somalia.
-
Al-Shabaab yateka mji wa kistratajia Somalia na kufunga viwanja 30 vya michezo
Jun 08, 2018 03:28Kundi la kigaidi na ukufurishaji la al-Shabaab limeteka mji moja wa kiistratajia karibu na eneo la Baidoa sambamba na kufunga viwanja zadi ya 30 vya michezo katika mji kuu Mogadishu.
-
UN yaunga mkono juhudi za kuleta utulivu Somalia
Jun 08, 2018 00:05Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi wake kutokana na kuongezeka ukosefu wa usalama na hali mbaya ya kibinadamu nchini Somalia na kusisitiza kuwa inaunga mkono juhudi za kuleta utulivu katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika iliyoharibiwa vibaya na vita vya ndani.