-
Kenya kuisaidia Somalia kuiumarisha mfumo wa sheria
Mar 09, 2018 03:18Mwanasheria mkuu wa Kenya, Githu Muigai amesema, nchi yake itaisaidia Somalia kuimarisha mfumo wake wa sheria, ili kukabiliana vizuri zaidi na na changamoto za kijamii na kisiasa.
-
Askari 5 wa AU miongoni mwa watu 16 waliouawa katika hujuma za al-Shabaab Somalia
Mar 04, 2018 04:46Imerifiwa kuwa, wanajeshi watano wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom ni miongoni mwa watu 16 waliouawa katika mashambulizi ya hivi karibuni ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab karibu na Mogadishu.
-
Ethiopia yanunua hisa za Bandari ya Berbera Somaliland
Mar 02, 2018 04:21Serikali ya Ethiopia imenunua asilimia 19 ya hisa za Bandari ya Berbera iliyoko katika Jamhuri iliyojitangazia uhuru ya Somaliland nchini Somalia.
-
Amisom: Tumekomboa 80% ya maeneo yaliyokuwa chini ya al-Shabaab Somalia
Mar 02, 2018 04:13Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom kimesema kimefanikiwa kukomboa asilimia 80 ya maeneo ambayo yalikuwa kwenye makucha ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab.
-
UN yasema itaendelea kuunga mkono mapambano dhidi ya al-Shabaab Somalia
Feb 25, 2018 11:59Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa sambamba na kulaani mashambulizi ya kigaidi ya hivi karibuni yaliyoua makumi ya watu katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, amesisitiza kuwa umoja huo utaendelea kuunga mkono jitihada za kulitokomeza kundi la kigaidi na la ukufurishaji la al-Shabaab.
-
Idadi ya watu waliouawa katika mripuko wa jana mjini Mogadishu Somalia yafikia 18
Feb 24, 2018 04:12Idadi ya watu waliouawa katika mripuko wa bomu mjini Mogadishu, Somalia imefikia 18.
-
Magaidi wanne watiwa mbaroni katikati ya Somalia
Feb 08, 2018 00:29Jeshi la Somalia limetangaza habari ya kutiwa mbaroni magaidi wanne wa genge la wakufurishaji la al Shabab, katikati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Jaji wa Somalia ateuliwa Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu ICJ
Feb 07, 2018 04:12Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu ICJ, yenye makao yake huko The Hague nchini Uholanzi imemteua Jaji Abdulqawi Ahmed Yusuf wa Somalia kuwa rais wake.
-
Mkuu wa Kamati ya Masuala ya Katiba Bunge la Somalia asema: Imarati ilipanga kumuua
Feb 03, 2018 23:12Mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Katiba ya Mabunge ya Somalia amesema kuwa vyombo vya ujasusi vya Imarati vilihusika na shambulizi lililolenga nyumba yake mjini Mogadishu mwishoni mwa mwezi Disemba na kwamba lengo la shambulizi hilo lilikuwa kumuua yeye.
-
Amisom: Huenda tusiondoe askari wetu Somalia kufikia 2020
Jan 28, 2018 04:20Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom kimetahadharisha kuwa huenda ndoto ya kuwaondoa maelfu ya askari wake katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika isitimie bila msaada wa dharura na uungaji mkono wa jamii ya kimataifa.