-
Jeshi la Somalia lakomboa eneo la mpakani kutoka kwa al Shabab
Sep 12, 2017 22:02Jeshi al Somalia limefanikiwa kukomboa eneo la mpaka wa nchi hiyo na Kenya lililokuwa limetekwa na wapiganaji wa kundi la kigaidi la al Shabab.
-
Watu sita wauawa katika hujuma ya kigaidi Beledweyne Somalia
Sep 10, 2017 09:54Watu wasiopungua sita wameuawa leo Jumapili baada ya gaidi mmoja kujiripua katika mkahawa ulioko nje ya ofisi ya kiserikali katika mji wa Beledweyne kati mwa Somalia.
-
Kundi la al-Shabaab la Somalia ladai kuua makumi ya askari Kismayu
Sep 03, 2017 03:04Kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab limedai kuwa limeua makumi ya askari wa Somalia karibu na mji wa bandari wa Kismayu mapema leo Jumapili.
-
Shambulio la bomu la al-Shabaab siku ya Iddi laua 12 Puntland, Somalia
Sep 02, 2017 03:05Watu 12 wameuawa katika shambulizi la bomu lililofanywa na genge la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia.
-
Serikali ya Somalia yakiri kuua raia katika operesheni ya pamoja na Marekani
Aug 31, 2017 09:23Serikali ya Somalia hatimaye imekiri kwamba raia 10 wa Kisomali waliuawa eti kimakosa katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na jeshi la nchi hiyo na askari wa Marekani Ijumaa iliyopita.
-
Somalia yakataa "rushwa" ya Saudia, yagoma kujiunga na nchi zinazoisusia Qatar
Aug 30, 2017 22:23Rais wa Somalia amekataa pendekezo la kupewa Euro milioni 68 lililotolewa na utawala wa Kifalme wa Saudi Arabia mkabala wa kujiunga na muungano wa nchi zilizokata uhusiano wao na kuisusia Qatar.
-
Wasomali wakataa kuzika watu wao mpaka serikali ikiri ilihusika na mauaji yao
Aug 27, 2017 10:09Familia za Wasomali zimekataa kuzika maiti za wapendwa wao 10 wakiwemo watoto watatu mpaka serikali ikubali kubeba dhima ya mauaji yao yaliyofanywa katika shambulio lililotekelezwa kwa msaada wa jeshi la Marekani.
-
Wanajeshi wa Marekani waua watoto 3 katika hujuma Somalia
Aug 26, 2017 03:21Raia wasiopungua 10, wakiwemo watoto watatu, wameuawa katika hujuma ya pamoja na Jeshi la Marekani na Jeshi la Somalia kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Watu 10 wauawa na wanamgambo wanaoungwa mkono na Marekani kusini mwa Somalia
Aug 25, 2017 23:25Serikali ya Somalia imetangaza habari ya kuuawa watu 10 ambao ni raia wa kawaida katika shambulizi la wabeba silaha kijiji cha Barire, jimbo la Lower Shebelle, kusini mwa nchi hiyo.
-
Wakimbizi 70,000 warejea kwa hiari Somalia kutoka Kenya
Aug 25, 2017 01:59Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limesema limewarejesha nyumbani wakimbizi 70,516 wa Somalia kutoka Kenya, tangu kazi hiyo ianze mwaka 2014.