-
Wasomali wakataa kuzika watu wao mpaka serikali ikiri ilihusika na mauaji yao
Aug 27, 2017 10:09Familia za Wasomali zimekataa kuzika maiti za wapendwa wao 10 wakiwemo watoto watatu mpaka serikali ikubali kubeba dhima ya mauaji yao yaliyofanywa katika shambulio lililotekelezwa kwa msaada wa jeshi la Marekani.
-
Wanajeshi wa Marekani waua watoto 3 katika hujuma Somalia
Aug 26, 2017 03:21Raia wasiopungua 10, wakiwemo watoto watatu, wameuawa katika hujuma ya pamoja na Jeshi la Marekani na Jeshi la Somalia kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Watu 10 wauawa na wanamgambo wanaoungwa mkono na Marekani kusini mwa Somalia
Aug 25, 2017 23:25Serikali ya Somalia imetangaza habari ya kuuawa watu 10 ambao ni raia wa kawaida katika shambulizi la wabeba silaha kijiji cha Barire, jimbo la Lower Shebelle, kusini mwa nchi hiyo.
-
Wakimbizi 70,000 warejea kwa hiari Somalia kutoka Kenya
Aug 25, 2017 01:59Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limesema limewarejesha nyumbani wakimbizi 70,516 wa Somalia kutoka Kenya, tangu kazi hiyo ianze mwaka 2014.
-
Mji wa Bariire Somalia wakombolewa kutoka mikononi mwa wanamgambo wa al-Shabab
Aug 21, 2017 09:33Jeshi na Somalia likishirikiana na kikosi cha kusimamia amani cha Umoja wa Afrika nchini humo AMISOM vimefanikiwa kuukomboa mji wa kiistratejia wa Bariire wa kusini mwa nchi hiyo uliokuwa ukidhibitiwa na wanamgambo wa kigaidi wa al-Shabab.
-
Serikali ya Somalia yayaonya mashirika na taasisi za fedha zinazoisaidia al Shabab
Aug 14, 2017 02:45Serikali ya Somalia imayaonya mashirika na taasisi za mawasiliano na za kifedha zinazohusika na usafirishaji wa fedha kwa ajili ya kundi la kigaidi na kiwahabi la al Shabab nchini humo.
-
Kamanda wa zamani al-Shabaab ajiunga na serikali ya Somalia
Aug 13, 2017 23:06Aliyekuwa Naibu Kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab na pia msemaji wa zamani wa genge hilo la ukufurishaji Mukhtar Robow Abu Mansur, amejisalimisha kwa jeshi la nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Watu 20 wauawa katika mapigano yaliyowahusisha ash-Shabab wasiokubaliana Somalia
Aug 10, 2017 23:43Watu 20 wanaripotiwa kuuawa katika mapigano yaliyotokea kati ya wanachama wa kundi la ash-Shabab huko kusini magharibi mwa Somalia.
-
KDF yashambulia ngome za al-Shabaab karibu na Afmadow, Somalia
Aug 10, 2017 10:15Ndege za Jeshi la Ulinzi la Kenya KDF zimeshambulia ngome za kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika eneo la Weelmarow karibu na wilaya ya Afmadow, eneo la Lower Juba, kusini mwa Somalia.
-
Askari 7, raia 1 wauawa katika mashambulizi ya mabomu Somalia
Aug 06, 2017 03:10Kwa akali askari saba wameuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika mashambulizi ya mabomu yalilolenga msafara wa magari ya jeshi karibu na mji wa Baidoa nchini Somalia.