-
Kenya yaakhirisha tarehe ya kufunga kambi ya Dadaab
Nov 16, 2016 10:16Kenya imerefusha muda wa kuwarejesha makwao wakimbizi wa Somalia walioko katika kambi ya Dadaab iliyoko kaskazini mashariki mwa nchi, ambayo ilitazamiwa kufungwa kikamilifu kufikia mwishoni mwa mwezi huu.
-
Jeshi la Somalia lakomboa eneo jengine kutoka kwa ash Shabab
Nov 16, 2016 04:22Jeshi la Somalia limefanikiwa kukomboa eneo jengine katikati mwa nchi hiyo kutoka mikononi mwa kundi la wakufurishaji la ash Shabab.
-
Rais wa Somalia: Maeneo mengi ya nchi yanakabiliwa na ukame
Nov 14, 2016 00:37Rais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia ameitaka jamii ya kimataifa kutuma misaada ya dharura katika maeneo yanayokabiliwa na ukame na baa la njaa nchini humo.
-
UN: Raia hawana makaazi na mapigano yanaendelea Galkayo, Somalia
Nov 13, 2016 13:07Karibu watu 90,000 katika mji wa Galkayo nchini Somalia wameendelea kubaki bila makaazi kutokana na kuzidi hali ya wasiwasi na mapigano ya mara kwa mara baina ya vikosi vya maeneo yanayojiendeshea masuala yao ya ndani ya Galmudug na Puntland.
-
AU na EU zatofautiana kuhusiana na ulipaji mishahara ya askari wa AMISOM
Nov 13, 2016 04:51Umoja wa Afrika umekosoa vikali uamuzi wa Umoja wa Ulaya wa kuwalipa mishahara askari wa Burundi wanaohudumu katika kikosi cha kusimamia amani cha AU nchini Somalia AMISOM.
-
Baraza la Usalama kushirikiana na serikali ya Somalia dhidi ya uharamia
Nov 10, 2016 10:16Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesisitiza kuendeleza ushirikiano na serikali ya Somalia katika kupambana na uharamia.
-
Makumi wauawa katika mapigano mjini Galkayo, Somalia
Nov 08, 2016 03:52Watu karibu 30 wameuawa na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa katika mapigano mapya yaliyozuka kati ya vikosi vya majimbo mawili hasimu yenye mamlaka ya ndani nchini Somalia.
-
Al Shabab wadai kuripua bomu karibu na bunge la Somalia
Nov 06, 2016 12:02Kundi la kigaidi la al Shabab limedai kuhusika na hujuma ya bomu la kutegwa garini karibu na bunge la Somalia mjini Mogadishu ambapo wanajeshi wawili wa Kisomali waliuawa na wengine watano kujeruhiwa.
-
UN: Al Shabab ingali tishio kubwa kwa Somalia, Afrika Mashariki
Nov 05, 2016 01:04Magaidi wakufurishaji wa kundi la Al Shabab wametajwa kuwa tishio kubwa sana kwa nchi ya Somalia na eneo zima la mashariki mwa Afrika.
-
Somalia na UN zakaribisha usitishaji mapigano baina ya Puntland na GalMudug
Nov 05, 2016 00:05Rais wa Somalia na mjumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya nchi hiyo wamekaribisha makubaliano ya usitishaji mapigano yaliyofikiwa baina ya majimbo mawili ya nchi hiyo ya Puntland na GalMudug juu ya eneo la Galkayo.